Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Friday, October 3, 2014

JIONEE MWENYEWE HALI ILIVYOKUWA KATIKA BIRTHDAY PARTY YA MKALI DIAMOND PLATINUMZ, NAYE KAMA WEMA APEWA ZAWADI YA NDINGA











Picha: Ndani ya Birthday Party ya Diamond Platinumz na zawadi ya BMW aliyopewa














Watu wakiserebuka




Gari aina ya BMW alilopewa kama zawadi na Manegement yake

Mama Diamond akiwa ndani ya ndinga

PICHA KWA MSAADA WA TIMES FM $ MATUKIO TZ

Thursday, October 2, 2014

PITIA VICHWA VYA HABARI MAGAZETI YA LEO, KURASA ZA MBELE NA NYUMA, BILA KUSAHAU MAGAZETI YA UDAKU

3_76144.jpg

03_347ee.jpg

6_e20f7.jpg

4_10a18.jpg

5_af5ec.jpg

7_33608.jpg

70_e6363.jpg

71_b991a.jpg

KURASA ZA NYUMA, HABARI ZA MICHEZO

32_06774.jpg

30_75973.jpg

35_222a4.jpg

33_9f670.jpg

36_218a2.jpg

22_c104c.jpg

23_571f8.jpg

20_15cd1.jpg
21_b0f75.jpg

37_e1a91.jpg

60_f95c7.jpg

61_1213b.jpg

 PATA HABARI ZAIDI HAPA

JOHN MNYIKA: MAHARAMIA WAMEPITISHA KATIBA HARAMU


Dira ni kuwa na katiba bora itakayojenga Tanzania yenye demokrasia ya kweli, uhuru wa kweli na maendeleo endelevu kwa watu wake wote. Lakini uharamia katika mchakato wa katiba mpya umelipasua taifa. Mpasuko huu unaweza kuwa mgogoro hasi wenye madhara kwa wananchi au mgogoro chanya utakaoleta mabadiliko nchini.
Maharamia wanashangilia kilevi katika Bunge Maalum baada ya kukamilisha uharamia dhidi ya rasimu ya katiba ya wananchi kwa kupata theluthi mbili kwa njia za kiharamia. Katiba iliyopendekezwa kiharamia na kudharau maoni ya wananchi ni katiba haramu iliyokosa maridhiano na muafaka wa kitaifa.
Katiba haramu, katiba ya maharamia, katiba ya mafisadi, katiba ya CCM wahafidhiana na mawakala wake inapaswa kupingwa mtaani na mahakamani kwa mbinu mbalimbali.
Iwe ni kwa mikutano, migomo, maandamano, mashtaka au katika sanduku la kura. Namshukuru Mwenyezi Mungu kwamba mchakato huu wa mabadiliko ya katiba ni mwanya wa mabadiliko katika taifa letu.
Theluthi mbili ilianza kutafutwa tangu wakati wa kutungwa kwa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, tulipinga muundo wa Bunge Maalum na uteuzi wake; madhara yake yamedhihirika sasa.
Rais Kikwete akaongezea udhaifu huo kwa kutumia madaraka vibaya kuteua wanaCCM mahafidhina na mawakala wao kwa wingi katika uteuzi wa wajumbe wa kundi la 201 kuongezea katika hodhi haramu ya wabunge na wawakilishi wa chama chake.
Sitta akakamilisha uharamia huo kwa marekebisho haramu ya kanuni za Bunge Maalum ambayo yaliruhusu kura kupigwa nje ya Bunge hilo na mianya mingine ya wizi wa kura.
Jana Oktoba Mosi Sitta alilalamikia hatua yangu ya kumtaja yeye, Chenge na wenzake kuwa ni ‘maharamia’ dhidi ya rasimu iliyotokana na maoni ya wananchi. Kwa kuwaita maharamia Sitta amelieleza Bunge Maalum kuwa ni “siasa za kichuo chuo” na kwamba “hatuwezi kushika madaraka kwa mbinu za kitoto”.
Nimkumbushe Sitta na maharamia wenzake kwamba mwaka 1958 Mwalimu Julius Nyerere alishtakiwa kwa kuwaita ‘mashetani na maharamia’ wakuu wa wilaya wa Serikali ya mkoloni. Ninapolitazama Bunge Maalum nakumbuka utetezi wake mahakamani wa kukiri kutamka maneno hayo kwa lengo la kuitaka serikali ya kikoloni itupie macho malalamiko ya watu.
Sitta na maharamia wenzake kama wameshindwa hata kuelewa waraka wa viongozi wa dini na kuuita kuwa “hauna utukufu wa Mungu na wa kipuuzi”, ni wazi wamelewa madaraka wasaidiwe kwa kupumzishwa.
Leo Sitta, Samia Suluhu na maharamia wengine wanasherehekea kama walevi ushindi wa muda mfupi walioupata kwa njia za kiharamia ikiwemo kwa kuwashinikiza na kuwarubuni baadhi ya wajumbe kuhalalisha rasimu haramu. Andrew Chenge aliyetajwa kwenye orodha ya mafisadi (list of shame) ndiye aliyeongoza kazi hiyo kuanzia katika Kamati ya Uandishi.
Uharamia huu dhidi ya rasimu ya tume ya mabadiliko ya katiba na maoni ya wananchi unapaswa kuwa kiunganishi kwa umma kutambua kwamba umoja wa ukweli na uadilifu unapaswa kuvuka mipaka ya vyama, dini, pande mbili za Muungano na tofauti zingine.
Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) umeonyesha msimamo wake, Mwenyekiti na Wajumbe wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba wameonyesha msimamo wao, baadhi ya viongozi wa dini wameonyesha msimamo wao, baadhi ya wanaharakati wameonyesha msimamo wao, baadhi ya wajumbe ndani ya Bunge Maalum wameonyesha msimamo wao; wewe je?
Namna pekee ya kuirejesha rasimu ya katiba ya wananchi katika hali iliyofikia ni kuikataa katiba haramu na kuwakataa wote waliofanya uharamia kuwezesha rasimu hiyo kupendekezwa na wote watakao itetea katiba hiyo.
Muasisi wa CCM alikiambia chama hicho mwaka 1995 kwamba “watanzania wanataka mabadiliko wasipoyapata ndani ya CCM, watayatafuta nje ya CCM”. CCM imepoteza mwanya wa kuwapa watanzania mabadiliko kutoka ndani ya chama hicho.
Uharamia uliofanywa katika Bunge Maalum una baraka za Katibu Mkuu wa CCM Kinana na Mwenyekiti wa CCM Rais Kikwete. Uharamia huo ulilenga kuwezesha Maoni ya CCM yaliyopitishwa na vikao vya juu vya CCM kinyume na maoni ya wananchi. Hatimaye kwa njia za kiharamia wajumbe wanaojiita walio wengi wa CCM wamepitisha katiba haramu iliyopendekezwa.
Mwalimu Nyerere aliandika katika kitabu cha Uongozi Wetu na Hatma ya Tanzania kwamba Rais wa wakati huo Mwinyi alikuwa mtu mwema na mpole lakini “kiongozi dhaifu”. Akamtakia heri na kuomba asaidiwe amalize kipindi chake salama. Akatabiri kwamba chini ya CCM na uongozi wake mbele ni giza tororo.
Rais Kikwete alithubutu kwa kukubali mchakato wa mabadiliko ya katiba kuanza lakini ameshindwa. Na kwa udhaifu alio uonyesha, kwa vyovyote vile mchakato huu hauwezi kusonga mbele na kukamilika chini yake.
Udhaifu pekee anao weza kuupunguza kwa sasa ni kusimamia marekebisho ya 15 ya Katiba ya mwaka 1977 kuwezesha uchaguzi huru na haki katika uchaguzi mkuu wa udiwani, ubunge na urais mwaka 2015 na kuendelea kwa mchakato wa katiba mpya mwaka 2016 kwa kuzingatia maoni ya wananchi. Tumtakie heri Rais Kikwete amalize kipindi chake salama; matokeo ya kura ya katiba haramu iliyopendezwa yatafutwa kwa kupingwa mahakamani ama kwa njia nyingine.
Mahakama kwa kukosa uhuru wa kikatiba isipotimiza wajibu huo wa kusimamia haki kwa wakati; katiba haramu iliyopendekezwa itafutwa kwa sheria maalum itayotungwa na Bunge litakaloongoza nchi baada ya uchaguzi 2015. Ikiwa watawala wa sasa au wa wakati huo watalazimisha katiba haramu kwenda kupigiwa kura ya maoni, ni wazi itapigiwa kura ya hapana na wananchi iwe ni mwaka 2015 au 2016.
Mabadiliko yatafutwe kwa kuwakataa watetezi wote wa katiba haramu kuanzia kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji mwaka 2014. Mabadiliko yatafutwe kwa kutaka Tume itangaze ratiba ya uandikishaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura mwaka 2014 ili kila mwenye umri wa kupiga kura ashiriki kufanya mabadiliko kupitia uchaguzi 2015 na kura ya maoni.
Kwa wajumbe mlioshiriki kuandika katiba haramu, naheshimu na nakubaliana na maneno ya Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji (Mstaafu) Joseph Warioba kwamba tutakutana mtaani. Dhima ni kuwa na katiba mpya itayoleta uongozi bora, sera sahihi, mikakati makini na Muungano na Muundo wa Utawala thabiti kwa maendeleo endelevu. Nyinyi mkiwa na katiba haramu sisi tutakuwa na rasimu ya wananchi; sauti ya watu, ni sauti ya Mungu hivyo umma utaamua na historia itatoa hukumu kwa maharamia na walevi wa madaraka.

Tuesday, September 30, 2014

FACEBOOK YAPATA MPINZANI, WADAU WAUBATIZA ANTI-FACEBOOK

Mtandao wa kijamii wa Ello unapokea maombi 31,000 ya watumiaji wanaotaka kujiunga kila saa moja hali ambayo inaibua ushindani mkubwa kwa mtandao wa Facebook.

Muanzilishi wa mtandao huo Paul Budnitz ameiambia BBC kuwa wakati mtandao huo unaazishwa ulilenga watu kuhudumia marafiki 90 tu.

Mtandao huu kwa mjibu wa muanzilishi umeanzishwa August mwaka huu ukiwa ambapo hauna gharama yoyote kwa mtumiaji iwe matangazo ama kulipia data.
Hata hivyo baadhi ya watumiaji wameubatiza kwa jina la Anti-Facebook mtandao huo, wakimaanisha kwamba ndiye mpinzani mkubwa wa Facebook.

Baadhi ya wataalam wa masuala ya kimitandao wamekosoa mfumo wa Ello kutotoza gharama yoyote wakidai kuwa katika siku za usoni huenda mtandao wa Ello utalazimika kutoza kiasi kidogo cha fedha kwa watumiaji wake.

Paul Budnitz mtengenezaji wa baiskel za kampuni ya Vermont ameiambia BBC kuwa wapo imara katika ushindani wa kimitandao na kujigamba kuwa ana wataalamu wa kutosha kukabiliana na makampuni pinzania.

Hata hivyo kuhusiana na baadhi ya watu kuuiita kwa jinala bandia la anti-Facebook mtandao huo yeye amesema wanajiendesha kama mtandao wenye mtazamo wake binafsi na si kutegemea mtazamo wa mtandao wa Facebook.
CHANZO BBC

Tuesday, September 23, 2014

HIVI NDIVYO TULIVYOSHEREHEKEA KATIKA BIRTHDAY YA MTOTO WETU DAVID

My son, David alizaliwa tarehe 22/09/2013, mwezi huu wa 9, tarehe 22 alikuwa ndo anafunga mwaka, hivyo kama wazazi tuliamua kuandaa chakula cha jioni ili kujumuika na ndugu, marafiki na jamaa zetu ili kwa pamoja tuweze kuadhimisha siku hii muhimu katika familia yetu. Kwa ndugu, jamaa na marafiki ambao hawakuweza kufika kutoka na umbali au matatizo ya hapa na pale ambao walipenda wajumuike nasi lakini haikuwezekana, tumuona tuwaletee tukio zima katika picha, basi jumuika nasi kwa kuangalia picha hizi


 David na mama yake

                Baba D.


 Mwabeza akisoma neno la Mungu




 Baba David akiwakaribisha wageni


 Mama David akiwapungia mkono wageni 


 Mr. Prosper, ndiye alikuwa Dj. wa shughuli yenyewe


                                                                                       








 David akimlisha keki yake wa baba wa ubatizo, John Kimolo
         David akimlisha keki mama yake

   Akimmlisha keki baba yake

 Akimlisha keki bibi yake

 Akimlisha keki baba Enosh, (Mwl. Mwabeza)

















  Hii ndo familia, mama, dady, son












Tunakuombea kwa Mungu mtoto wetu David,uendelee kukua vizuri, akupe maisha mazuri na marefu, wazazi wako tunakupenda sana. Mungu akulinde.

Tunapenda kuwashukuru wote waliohudhuria katika shughuli ya kumpongeza mtoto wetu kwa kutimiza mwaka mmoja. Janeth Lubasi, Boniface Manyasa, Steven Mandia, familia ya Mwabeza, familia ya Madata, Moris Nyamwale, familia ya John Kimoro, familia ya Gwamaka, Sarah Mgulula, Maria Ntandu, Edward Mbuya, John Maghway, Mama Schola, Sylvery Hussein, Stewart Prosper, Elizabeth, Agnes, n.k. Tunawashukuru hawa wote kwa kuweza kutupa kampani ya kutosha katika siku hii muhimu ya mtoto wetu kutimiza mwaka mmoja. Mungu awabariki sana na awazidishie pale walipopungukiwa.

Familia ya Mr. & Mrs Furaha Venance Kaguo