Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Wednesday, February 18, 2015

RAIS KIKWETE APANGUA WAKUU WA WILAYA, WAPYA WAINGIA WENGINE WAACHWA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

UTEUZI WA WAKUU WA WILAYA FEBRUARY 18, 2015

Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, amefanya mabadiliko ya Wakuu wa Wilaya ili kuboresha utendaji kazi. Mabadiliko hayo yamezingatia kuwepo kwa nafasi wazi ishirini na saba (27) zilizotokana na:
  1. Kufariki dunia Wakuu wa Wilaya 3
  2. Kupandishwa cheo Wakuu wa Wilaya 5 kuwa Wakuu wa Mikoa
  3. Kupangiwa majukumu mengine Wakuu wa Wilaya 7; na
  4. Kutengua uteuzi wa Wakuu wa Wilaya 12
Katika mabadiliko hayo, Mheshimiwa Rais amewateua Wakuu wapya wa Wilaya 27 ili kujaza nafasi hizo wazi.
Aidha, Wakuu wa Wilaya sitini na nne (64) wamebadilishwa vituo vya kazi na Wakuu wa Wilaya arobaini na mbili (42) wameendelea kubaki katika vituo vya sasa.

No comments:

Post a Comment