Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Thursday, September 13, 2018

HAYA NDIYO MATAIFA 38 "YANAYOAIBISHA DUNIANI"


 Katibu Mkuu Antonio Guterres

Umoja wa Mataifa Jumatano umetaja mataifa 38 "yanayo aibisha" yakiwemo China na Russia kwa kile walichodai kuwa ni ulipizaji kisasi au vitisho dhidi ya wale wanaoshirikiana na umoja huo kwa ajili ya kuchunguza ukiukaji wa haki za binadamu.

Miongoni mwa unyanyasaji ulotajwa ni pamoja na mauaji, mateso na kukamatwa kiholela kwa watu hao.

Ripoti ya kila mwaka iliyotolewa na Katibu Mkuu wa UN Antonio Guterres imetaja pia kuwepo na kampeni kuwafuatilia, kuwatendea maovu, na kuwaaibisha hadharani watetezi wa haki za binadam na waathiriwa.

Mataifa hayo 38 yanajumuisha 29 yenye kesi mpya na mengine 19 yakikabiliwa na kesi zinazoendelea.

Ripoti inaeleza kwamba mataifa mengi yanadaiwa kuwafungulia mashtaka wanaharakati wa haki za binadamu kwa ugaidi au kushirikiana na mataifa ya kigeni kuhujumu hadhi na usalama wa taifa, ikiwa ni njia ya kuwatishia wasiendelee kushirikiana na UN katika uchunguzi huo.

Kesi hizo mpya zinazochunguzwa ziko Bahrain, Cameroon, China, Colombia, Cuba, DRC, Djibouti, Misri, Guatemala, Guyana, Honduras, Hungary, India Israel, Krygyszstan, Maldives.

Nyingine ni Mali Morocco, Myanmar. Ufilipino, Rwanda. Saudia Arabia, Sudan Kusini, Thailand, Trinidad na Tobago, Uturuki, Turkmeni na Venezuela.

Chanzo: VOA

Thursday, May 24, 2018

ORODHA YA MAJINA YA VIJANA WALIOHITIMU KIDATO CHA SITA MEI 2018 KWA AJILI YA KUHUDHURIA MAFUNZO YA MUJIBU WA SHERIA



 TAARIFA KWA UMMA

Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), limefanya uteuzi wa wanafunzi waliohitimu elimu ya sekondari kidato cha sita kutoka shule zote za Tanzania Bara kwa mwaka 2018, kuhudhuria mafunzo ya JKT kwa mujibu wa Sheria.

Sanjari na uteuzi huo, JKT limewapangia Makambi ya JKT watakayokwenda kupatiwa mafunzo kwa muda wa miezi mitatu na wanatakiwa kuripoti makambini kuanzia tarehe 01-10 June 2018.

Wahitimu hao, wamepangiwa katika Kambi za JKT Rwamkoma – Mara, JKT Msange – Tabora, JKT Ruvu – Pwani, JKT Makutupora – Dodoma, JKT Mafinga – Iringa, JKT Mlale – Ruvuma, JKT Mgambo na JKT Maramba – Tanga, JKT Makuyuni – Arusha, JKT Bulombora, JKT Kanembwa, Nachingwea- Lindi na JKT Mtabila – Kigoma.

Aidha, wahitimu wenye ulemavu wa kuonekana kwa macho (physical disabilities) wanatakiwa kuripoti kambi ya Ruvu JKT iliyopo mkoani Pwani ambayo ina miundombinu ya kuhudumia wa jamii hiyo.

Vijana watakaochaguliwa watatakiwa kujigharamia nauli za kwenda na kurudi kwenye makambi ya JKT waliyopangiwa wakiwa na vifaa vifuatavyo:

  1. Bukta ya rangi ya Dark blue yenye mpira kiunoni (lastic), iliyo na mfuko mmoja nyuma, urefu unaoishia magotini isiyo na zipu. Aidha bukta za wanawake zinatakiwa kuwa na lastic magotini.
  2. Raba za michezo zenye rangi ya kijani.
  3. Shuka mbili za kulalia zenye rangi ya blue bahari.
  4. Soksi ndefu za rangi nyeusi.
  5. Nguo za kuzuia baridi kwa waliopangwa kwenye mikoa yenye baridi.
  6. Track Suit ya rangi ya kijana au bluu

Mkuu wa JKT anawakaribisha vijana wote walioteuliwa ili waweze kujiunga na vijana wenzao katika kujifunza Uzalendo, Umoja wa Kitaifa, stadi za kazi, stadi za maisha na Utayari wa kulijenga na kulitumikia Taifa letu.

KUTAZAMA MAJINA BOFYA LINK ZIFUATAZO KWA KILA KAMBI 


Endeleo kutembelea blog yetu tutakujuza zaidia.

Ingia hapa youtube chenel yetu SUBSCRIBE kupata taarifa zaidi

 Rayvanny 'Pochi Nene Remix' 
sikiliza verse ya Billnass iliyoondolwa kwenye remix hiyo.

Wednesday, April 11, 2018

VIDEO--MAGUFULI AMWAMBIA KIKWETE HATAONGEZA HATA DAKIKA 1 MADARAKANI MUD...


UTAFITI ULIWAHI KUBAINI KUWA WATANZANIA WANA IQ NDOGO.

Image may contain: 2 peopleKada wa CCM ajulikanae kwa jina Thadei Ole Mushi ameandika hivi kuhusiana na uwezo wa kufikiri kati ya Watanzania, Wakenya na Waganda. Soma makala haya kisha shusha comment yako chini unakubaliana nae kwa asilimia ngapi?

Na Thadei Ole Mushi.
Kuna utafiti uliwahi kusema kuwa sisi watanzania tuna IQ ndogo kuliko nchi zote za Afrika mashariki. Walidai kwenye swala la Abstract reasoning ni wa mwisho kabisa...... na concur observation hiyo hebu ona:- 

#Nchini Kenya:- Wananchi wanafuatilia kwa karibu sana Mijadala inayoendelea Bungeni na mijadala iliyopo viral ni swala la Ajira kwa vijana, Kilimo na Uwekezaji. Wananchi wanajadili kila kona yanayoendelea Bungeni tafsiri yake ni kuwa Bunge linapata uhai nje na ndani. Wananchi wanaongeza pressure kwenye mambo ya msingi.

Kiuchumi huku njee wanajadili uwekezaji mkubwa wa uanzishwaji wa viwanda vya kuassemble magari vinavyotaka kuanza kujengwa Nchini humo. Nafikiri hata Sisi Watanzania tumejikuta tunatekwa na mijadala ya Kenya.

#Nchini Uganda:- Bunge linaendelea kilichoshika kasi huko ni Bajeti ya wizara ya Kilimo wananchi na wabunge wamengangania iongezwe. Wanajadili makubaliano ya Kilimo ya Msumbiji yafuatwe kama yalivyo. Wananchi wanalipa bunge pressure toka njee na kweli bunge linapata uhai.

#Tanzania:-Asilimia 95 hawajui ni mijadala gani inaendelea Bungeni. Hakuna pressure yoyote ya maana toka kwa wananchi inayoongeza value kwenye Bunge letu. Mwananch Communication wasiporekodi ka clip hatuwezi kujua ni mijadala gani mizito inayotakiwa wananchi waijengee attention na kuiongezea pressure kwa manufaa ya kitaifa.

Kilichobamba huku njee ni mama mtu Mzima kudai kuwa yeye ni Mtoto wa Lowassa taifa Zima limehamia kwenye mjadala huo.

Kila mpango na Sera ya nchi uwe mbovu au mzuri unapigwa mhuri na Chombo hiki. Ukishatoka Bungeni unakwenda kwenye utekelezaji. Huku njee tunajadili mambo mepesi sana.
Hii ndio Tanzania tuna tatizo la msingi mahali.....
Morning Tanzania ngoja tuingie mzigoni kulijenga Taifa.

Ole Mushi.
0712702602

Unakubaliana nae kwa asilimia ngapi?

KAMA WEWE NI MTUMISHI WA UMMA KUPATA SALARY SLIP YAKO YA KILA MWEZI ONLINE

Monday, March 5, 2018

CAMFED YASHUSHA NEEMA KWA WANAFUNZI WA MWANZI. YAGAWA BAISKELI KIBAO NA VIFAA VINGINE



                            
                                                                                    Na. Mwl. Venance. F.K.
Shirika linalowasaidia wanafunzi wa kike litwalo CAMFED limetoa msaada wa baiskeli na mahitaji mengine kama vile magodoro, sale za shule, taulo za akina mama, madaftari, taa za sola na viatu vya shule. Aidha wapo wengine waliopata pesa kwa ajili ya kulipia pango na matumizi.
Akizungumza katika makabidhiano mbele ya wazazi na wageni waalikwa hapo jana (tar. 05/03/2018) Mkuu wa Shule Janeth Lubasi alisema wanafunzi takribani 60 ndiyo wanafadhiliwa na shirika hilo. Ambao kwa utaratibu kila mwaka wanafunzi wanajaza fomu maalumu kuomba ufadhili kwa kuandika mahitaji wanayoyahitaji kwa mwaka mzima. Kila mwanafunzi alitakiwa kuomba mahitaji ya kiasi kisichozidi Tsh. 250,000/=.

“Kati ya wanafunzi 60 wanafunzi 47 waliomba kununuliwa baiskeli, hivyo wazazi msishangae kuona wanafunzi wengine wanapata baiskeli wengine hapati…kila mwanafunzi amepewa kile alichoomba.” Alisema mkuu wa shule.

Aidha aliwataka wazazi kuzingatia kuwa vifaa hivyo ni kwa ajili ya wanafunzi walengwa tu na si vya wazazi. “Hatutegemei kumkuta mzazi mnadani akiwa na baiskeli ya motto…baiskeli hii ni kwa ajili ya motto tu…na wazazi ambao watoto wao wamepewa magodoro hairuhusiwi mzazi kumbadilishia motto kudoro au kulichukua na kulitumia nyie…” alisema mkuu wa shule. 

Kabla ya kumkaribisha Mbunge wa Manyoni Mashariki, Mh. Daniel Mtuka, diwani wa kata ya Manyoni, Mh. Machibula aliwataka wanafunzi hao kuwa mabalozi wazuri kwa wenzao na kuhakikisha wanasoma kwa bidii.

Mbunge wa Manyoni Mashariki Daniel Mtuka alisema kuwa ni jambo la kujivunia sana shule ya Mwanzi kuwa miongoni mwa shule zinazofadhiliwa na Camfed. “ndani ya mwanamke kuna kitu…ndiyo maana hawa CAMFED wameona umuhimu wa kuwasaidia hawa watoto wa kike…jambo la muhimu hivi vifaa vitusaidie katika kufanikisha malengo yetu ya elimu watoto” alisema.

Aidha mmoja wa wazazi ambaye mwandishi wetu alishindwa kupata jina lake alitoa neno la shukrani kwa niaba ya wazazi, aliushukuru sana uongozi wa shule na CAMFED kwa kuamua kuwasaidia.
jamani sisi wengine hata uwezo wa kununua viatu pea mbili hatuna…leo tumekabidhiwa baiskeli, viatu na vitu vingine tunasema asante asante sana yaani tunasema asante zaidi ya asante yenyewe.” Alisema.

Nisikuchoshe ungana na mwandishi wetu katika matukio katika picha hapa chini:



 Mh. Diwani wa Kata ya Manyoni akitoa salamu zake


Mh. Mbunge wa Jimbo la Manyoni Mashariki 
akimkabidhi mmoja wa wanafunzi vifaa


Baadhi ya baiskel walizopewa wanafunzi

 Mmoja wa wazazi ambaye mtoto wake ni mnufaika wa Camfed 
akitoa neno la shukrani

 Mmoja wa wanafunzi akipatiwa godoro na vifaa vingine na Mh. Mbunge

 Mwenyekiti wa Bodi ya Shule, Mzee Msongo akitoa neno siku hiyo


Picha zimepigwa na Baba D.

Tuesday, January 30, 2018

WILAYA YA MANYONI: UFAULU WA SHULE ZA WILAYA YA MANYONI KIMADARAJA




 Tokeo la picha la necta

WILAYA YA MANYONI

UFAULU WA SHULE ZA WILAYA YA MANYONI KIMADARAJA



SN
SHULE
DIV. I
DIV. II
DIV. III
DIV. IV
FLD (ZERO)
1
ITIGI
O
10
19
50
29
2
MWANZI
1
6
16
47
24
3
MANYONI
0
3
11
52
22
4
KILIMATINDE
1
2
3
33
18
5
HEKA
0
1
2
12
15
6
KINTIKU
0
3
5
18
5
7
MAKURU
0
5
5
11
11
8
NKONKO
0
2
2
13
1
9
KIMADOI
1
1
12
53
21
10
MKWESE
0
1
4
8
7
11
AMANI GIRLS
14
52
19
2
0
12
ST. JOHN
3
27
20
2
0
13
RUNGWA
0
0
0
6
4
14
IDODYANDOLR
0
0
2
6
8
15
KINANGALI
0
4
5
3
5
16
NGAITI
1
0
4
11
5
17
IPAMUDA
0
0
1
2
4
18
ISSEKE
0
0
3
2
0
19
MAKANDA
0
0
3
3
2
20
SANZA
0
0
2
9
10
21
KIZIGO
2
2
4
10
3
22
SASAJILA
0
0
1
3
3
23
KAMENYANGA
 1
0
6
22
8
24
SANJARANDA
0
11
9
24
7




























25
CHIKUYU
0
0
2
15
17



26
MITUNDU
0
2
5
33
11
27 MGANDU 0 2 1 17 12








28
MLEWA
0
0
1
24
33




BOFYA KATIKA SHULE UITAKAYO HAPA CHINI KUANGALIA MATOKEO

1.       MANYONI SECONDARY SCHOOL
5.       SASAJILA SECONDARY SCHOOL
6.       ITIGI SECONDARY SCHOOL
8.       HEKA SECONDARY SCHOOL
9.       KINTINKU SECONDARY SCHOOL
14.   AMANI GIRLS

SHULE NYINGINE ZA MANYONI TUTAINGIZA MATOKEO YAKE HIVI PUNDE