Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Thursday, January 30, 2014

VITA YA URAIS 2015 CCM, NI PIGA NIKUPIGE, YAWAIBUA WAANZILISHI WA CCJ NDANI YA CCM

 Richad KiaboMALUMBANO ya makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) yanayoonekana dhahiri kuchagizwa na makundi ya urais yameendelea kushika kasi ndani ya chama hicho.
 
Baada ya jana Katibu wa Uhamasishaji na Chipukizi, Paul Makonda, kumshambulia Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, kwamba anawatumia watu kusema hovyo kupitia vyombo vya habari juu ya kazi na juhudi zinazofanywa na sekretarieti, kada mwingine, Richad Kiabo, jana aliibuka kuanika majina ya waasisi wa chama cha siasa cha CCJ kilichokufa hata kabla ya kupata usajili.
 
Makonda alidai Lowassa anafadhili mikakati ya kupingana na juhudi za sekretarieti ya chama hicho na alipongeza kazi zinazofanywa na sekretarieti chini ya Katibu Mkuu, Abdulrahaman Kinana na wasaidizi wake akiwemo Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye.
 
 
Akizungumza na waandishi wa habari jana, akijibu mapigo ya Makonda, Kiabo aliyekuwa mwenyekiti wa CCJ kabla ya kurejea CCM, aliyataja majina 37 na michango waliyoitoa kwa ajili ya kufanikisha maandamano ya amani ya chama hicho ya kupinga uonevu wa aliyekuwa msajili wa vyama vya siasa nchini wakati huo, John Tendwa.
 
Kiabo ambaye amekoleza malumbano hayo, alimtaka Makamu Mwenyekiti wa CCM, Philip Mangula, kuwachukulia hatua wasaliti hao.
 
Mbele ya waandishi wa habari, Kiabo aliwataja waasisi hao wa CCJ na fedha walizochangia kwenye mabano kuwa ni pamoja na Dk. Harrison Mwakyembe (sh 300,000), Samuel Sitta (sh 500,000), Anne Kilango (sh 400,000), Nape Nnauye (sh 100,000), Paul Makonda (sh 100,000) na James Lembel (sh 400,000) ambao kwa sasa ni miongoni mwa wanachama wa CCM wanaotajwa kuwa na makundi ya urais.
 
Wengine ni Amina Katemi (sh 300,000), Alex Kisumo (sh 300,000), Baraka Seif (sh 300,000), Sospeter Banigwa (sh 300,000), Saleh Omari (sh 300,000), Sarah Patrick (sh 200,000), Daniel Mwaijojeli (sh 200,000), Dk. Ngonyani (sh 300,000), Elisha Eliya (sh 200,000), Emanuel Magonja (sh 200,000) na Asma Watosha (sh 300,000).
 
Pia wamo, Kulwa Lulelema (sh 50,000), Hamadi Maduku (sh 100,000), Flavian Nkya (sh 100,000), Gulam kutoka Zanzibar (sh 150,000), Hamad Ferej (sh 200,000), Ally Harun (sh 50,000), Masudi Kangi (sh 100,000), Gumbo (sh 150,000), Idd Kiriwe (sh 100,000), Innocent Makala (sh 200,000), Jacob Msambya (sh 200,000), Ishelula (sh 150,000), Kipute (sh 200,000), Joseph Kashindye (sh 200,000) Kamala Ng’ombe (sh 200,000) na Daniel Malongo (sh 50,000).
 
 
Kiabo alisema anashangaa kuona ndani ya CCM bado kuna wanachama na viongozi waandamizi wenye kadi mbili, yaani kadi ya CCJ na CCM na wameshindwa mpaka sasa kuzirudisha na hata kukana, ikiwemo kuwaomba radhi wanachama kwa kitendo cha usaliti.
 
“Nawashangaa baadhi ya wanachama ambao si waaminifu na wasaliti wa chama baadhi yao wameanza harakati za kugombea urais 2015 ili wapewe ridhaa na chama ambacho tayari walikwisha kisaliti, nami nitakishangaa chama wakati ukifika kama kitawakubalia na kuwapitisha kuwa wagombea watu wenye kadi za vyama viwili,” alisema.
 
Kiabo alisema watu wenye uwezo wa kuwasema viongozi wenzao mara kwa mara na wao wasijisahau kuwa hawana usafi wowote wa kusema na kuwanyoshea vidole wenzao kwa usaliti walioifanyia CCM.
 
Aidha, alisema wakati CCM ikielekea katika uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu 2015 ni vizuri kikaanza kusafisha nyumba yake ili mamluki waumbuke na wasipewe nafasi ya kugombea wakati ukifika.
 
Kutoka jijini Morogoro, inaripotiwa kuwa UVCCM Mkoa wa Morogoro imemtaka Makonda kumwomba radhi Lowassa kwa kauli za kichochezi zinazoweza kukigawa chama.
 
Kwa mujibu wa taarifa iliyosambazwa katika mitandao ya kijamii jana, wajumbe hao wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) kupitia kundi la vijana, Jonas Nkya na Ramadhani Kimwaga, walisema kauli ya Makonda ni yake binafsi wala haihusiani na UVCCM.
 
Nkya alisema vijana wa Mkoa wa Morogoro wamehuzunishwa na matamshi ya Makonda akimshutumu Lowassa kuwa hafai kuwa kiongozi wa nchi hii, wala kuwa Amiri Jeshi Mkuu na Mwenyekiti wa CCM taifa.
 
Nkya alisema kuwa umoja huo hautaki kuingizwa katika masuala binafsi ambayo yanaweza kusababisha na kuchangia kukigawa chama na jumuiya zake.
 
Mnyukano wa sasa miongoni mwa makada wa CCM umekuja baada ya Rais Jakaya Kikwete kufanya uteuzi wa Baraza la Mawaziri na kuwarejesha madarakani mawaziri mizigo waliopendekezwa na chama chake watoswe.
 
Baada ya uteuzi huo, Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, alitoa kauli ya kuunga mkono uteuzi huo, lakini akisisitiza chama kitaendelea kuwashughulikia mawaziri mizigo na safari hii wataelekeza mapambano hayo ndani ya Bunge na kwenye mabaraza ya halmashauri.
 
Kauli hiyo ilimuibua mwenyekiti wa zamani wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita, ambaye alimtukana Nape kwamba ameteuliwa kimjombamjomba na hawezi kumchagulia rais majina ya uteuzi.
 
Kauli ya Guninita ikamuibua Makonda na sasa Kiabo, ambao duru za siasa zinasema wote wanatumiwa kwa malengo ya urais mwaka 2015
 
VIA: Tanzania Daima

Saturday, January 25, 2014

MAPYA! HITLER ALIKUFA MWAKA 1984 NA SI 1945, PICHA ZINATHIBITISHA


New book claims THIS picture proves Hitler escaped his Berlin bunker and died in South America in 1984 aged 95

  • Fuhrer 'fled to Argentina and then Paraguay before settling in Brazil'
  • Hunted for treasure with a map given to him by Vatican allies, book claims
  •  
  • Author Simoni Renee Guerreiro Dias claims fascist actually died aged 95
  •  
  • Claims he had a black girlfriend to disguise his fascist background
  •  
  • Says her suspicions increased after she photoshopped a moustache onto the grainy picture and compared it to photos of the Fuhrer

 
He is believed to have died after shooting himself in a Berlin bunker in 1945 when he realised Germany had lost World War II.

But a startling new book claims Adolf Hitler actually escaped his hideout and died incognito in 1984 in a small town near Brazil's border with Bolivia - and it can be proved by a picture.
 
Not only that, but the author believes the Fuhrer fled to Argentina and then Paraguay before settling in the Brazilian state of Mato Grosso to hunt for buried treasure - with a map given to him by Vatican allies, according to its author.
Simoni Renee Guerreiro Dias claims this picture proves Hitler lived in the small town of Nossa Senhora do Livramento with his girlfriend, Cutinga
Simoni Renee Guerreiro Dias claims this picture proves Hitler lived in the small town of Nossa Senhora do Livramento with his girlfriend, Cutinga
Old clothes meant to be worn by the Fuhrer: An author claims the fascist actually died aged 95
Old clothes meant to be worn by the Fuhrer: An author claims the fascist actually died aged 95
German Fuhrer Adolf Hitler 'went to Brazil to hunt for treasure'
German Fuhrer Adolf Hitler 'went to Brazil to hunt for treasure'
As part of his elaborate ruse to escape detection, he also had a relationship with a black woman called Cutinga, which was meant to prove that he could not be the dictator who hated anyone who did not fit his Aryan ideal, the book claims.

Post-graduate student Simoni Renee Guerreiro Dias has outlined her bizarre theory, claiming the fascist actually died aged 95.
The book, titled 'Hitler in Brazil - His Life and His Death', challenges the accepted view that the dictator shot himself in his Berlin bunker on April 30 1945.
She claims he may have lived as Adolf Leipzig in the small town of Nossa Senhora do Livramento, 30 miles from the state capital Cuiaba.
Simoni, a Brazilian who comes from Cuiaba, says Leipzig was known locally as the 'Old German.'
Simoni is now planning to use DNA tests using a relative of Hitler living in Israel, after been given permission to exhume Adolf Leipzig's remains from his alleged final resting place in Nossa Senhora do Livramento.
The journalism student has linked the Fuhrer's alleged arrival in the area to a Vatican offer of ownership rights over buried Jesuit treasure in a cave near his adopted home.
 

She points out in her book Leipzig was the birthplace of Hitler's favourite composer Bach.
Hitler's Bunker in the Chancellery, Berlin, where many believe he shot himself
Hitler's Bunker in the Chancellery, Berlin, where many believe he shot himself
The supposed burial site: The Fuhrer 'fled to Argentina and then Paraguay before settling in the Brazilian state of Mato Grosso'
The supposed burial site: The Fuhrer 'fled to Argentina and then Paraguay before settling in the Brazilian state of Mato Grosso'
 
 
She says her suspicions about Adolf Leipzig increased after she photoshopped a moustache on to the grainy picture she obtained of him and compared it to photos of the Nazi leader.

According to Simoni, an unidentified Polish nun recognised an elderly man due to have an op at a hospital in Cuiaba in the early eighties as Hitler and demanded he leave - but was reprimanded by a superior who claimed he was there on Vatican orders.
Academics in Brazil have also rubbished the theory Hitler lived and died in Nossa Senhora do Livramento.

THE CONSPIRACY THEORIES SURROUNDING HITLER'S DEATH

Conspiracy theorists have long argued Hitler escaped from Germany and fled to south America.
 
Authors Gerrard Williams and Simon Dunstan claimed in a 2011 book Grey Wolf: The Escape of Adolf Hitler, that the Fuhrer fled with his mistress Eva Braun to Patagonia and had two daughters before dying in 1962 aged 73.
 
The claims about Hitler's life in Argentina were ridiculed by historian Guy Walters, who described them as '2,000 per cent rubbish' when the book was published.
He added: 'It's an absolute disgrace. There's no substance to it at all. It appeals to the deluded fantasies of conspiracy theorists and has no place whatsoever in historical research.'
Candido Moreira Rodrigues, a history professor at Mato Grosso's Federal University said: 'There's nothing new in people who claim to be historians coming up with the most far-reaching theories about Hitler supposedly living in south America and subsequently dying in one of the countries in this region.'
 
Ten of thousands of Nazis escaped after the war, including the notorious Adolf Eichmann and Josef Mengele.
 
Investigators probing Hitler's demise were hampered by the lack of any physical evidence for his death.
 
Fantasists were given added ammunition he didn't die in his Berlin bunker when 2009 DNA tests on skull fragments found near the bunker, believed to be his, turned out to belong to a woman.
 
Rochus Misch, a former bodyguard of Adolf Hitler who has been named as the last man to see the Fuhrer alive during his final hours in Germany, died last September aged 96.
 
Misch, who lived with Hitler and his mistress in their underground refuge as the allies closed in, told before his death he saw Hitler slumped with his head on the table after hearing a gunshot behind his closed door.

Via : www.dailymail.co.uk

Sunday, January 19, 2014

SERIKALI YAWABEBA WALIOFELI KIDATO CHA PILI

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa. Picha na Maktaba

Dar es Salaam.
Wakati Watanzania wakisubiri matokeo ya kidato cha pili mwaka 2013, imebaini kuwa Serikali imetoa agizo kwamba wanafunzi wote waliofeli mtihani huo kuendelea na masomo ya kidato cha tatu, huku wakisoma mafunzo ya kurudia mtihani wa kidato cha pili.
 
 
Licha ya matokeo hayo kutotangazwa hadi sasa, imebainika kuwa waliofaulu mtihani huo uliofanywa Oktoba 7 hadi 21 mwaka jana ni asilimia 62 tu, asilimia 31 wakitakiwa kukariri (kurudia) kidato cha pili mwaka huu, huku asilimia saba wakishindwa mtihani huo kwa mara ya pili.
Jumla ya wanafunzi 531,457 walitajwa na Wizara ya Elimu mwaka jana kuwa watafanya mtihani huo.
 
Uamuzi huo wa Serikali ni tofauti na ule uliotolewa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa Novemba 4, mwaka 2012, kwamba kuanzia wakati huo mtihani wa kidato chapili utakuwa ni wa mchujo na kwamba atakayefeli atatimuliwa.
 
Dk Kawambwa alisema matokeo ya mtihani wa kidato cha pili yatatumika kama kigezo cha kuchuja na kukariri kidato cha pili kwa watahiniwa watakaoshindwa kufikia wastani wa ufaulu wa alama 30.
Alisema mtahiniwa ataruhusiwa kukariri kidato cha pili mara moja tu na endapo mtahiniwa atashindwa mtihani kwa mara ya pili kwa mwaka utakaofuatia, itabidi aendelee na elimu ya sekondari nje ya mfumo rasmi.
 
Gazeti hili limeiona barua iliyoandikwa Januari 16 mwaka huu na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na kusainiwa na Katibu Mkuu wake, Profesa Sifuni Mchome, kwenda kwa wadau wa elimu nchini, wakiwamo maofisa elimu wa mikoa na Chama cha Wamiliki wa Vyuo na Shule Binafsi (Tamongsco).
 
Katika barua hiyo, wizara hiyo imewataka wadau hao kuhakikisha kuwa wanafunzi watakaofeli mtihani huo, wanaendelea na masomo ya kidato cha tatu.
 
“Matokeo ya kidato cha pili yamepokewa na kufanyiwa uchambuzi ili kupata taswira ya taifa. Taarifa ya matokeo hayo imebaini kuwa watahiniwa waliofanya mtihani na kufaulu ni sawa na asilimia 62 tu,” inaeleza sehemu ya barua hiyo na kuongeza;
 
“Hali hii inaonyesha kuwa asilimia 31 ya wanafunzi watatakiwa kukariri kidato cha pili, 2014. Wale walioshindwa kwa mara ya pili ambao ni asilimia saba wanatakiwa kuendelea na masomo nje ya mfumo rasmi.”
 

Barua hiyo inaeleza kuwa wanafunzi waliofaulu kwa wastani wa alama 20 na kuendelea waendelee na masomo ya kidato cha tatu mwaka 2014, wakati awali Serikali ilitoa tamko kuwa watakaoshindwa kufikisha alama 30 watatimuliwa.
 
“Wanafunzi waliofaulu kwa wastani wa alama 20 hadi 39 wapewe mafunzo rekebishi ‘Remedial class’ wakiwa kidato cha tatu,” inaeleza sehemu ya barua hiyo.

Inaeleza kuwa uamuzi huo unawahusu wote wakiwamo wale walioshindwa kwa mara ya pili, “Kwa maana hiyo hakuna mwanafunzi atakayerudishwa nyumbani.”
 
Mwisho barua hiyo imewataka wadau hao kuhakikisha kuwa inawapa taarifa mameneja na wamiliki wa shule na seminari ili kusimamia utekelezaji wa uamuzi kuhusu matokeo hayo.
 
 
Kauli ya wizara
Akitolea ufafanuzi suala hilo, Profesa Mchome alisema, “Suala la wizara kuagiza wanafunzi wote waliofeli kuendelea na masomo ya kidato cha tatu mimi sijalisikia, ninachojua ni kwamba wapo watakaorudia.”
 
Alisema kuwa tayari wizara imeshapeleka taarifa za matokeo hayo na uamuzi wa Serikali katika kila kanda nchini. “Kila shule ina taarifa hizo. Wapo wanafunzi watakaorudia.”
 
 
Akizungumza kuhusu matokeo ya kidato cha pili mwaka 2013 kutotoka mpaka sasa alisema, “Ninachofahamu ni kwamba matokeo ya kidato cha pili yameshawasilishwa katika kanda zote nchini.”
 
 
“Unajua matokeo ya kidato cha pili siyo kama matokeo ya darasa la saba, kidato cha nne na sita. Matokeo ya kidato cha pili ni kama mwendelezo wa tathmini ‘Continuous assessment’ kwa mwanafunzi, hutumika pia katika mtihani wa kidato cha nne.”
 
Alisema ndiyo maana matokeo hayo hupelekwa katika shule husika. “Baada ya kupelekwa katika shule husika, hapo ndipo inaweza kutolewa taarifa za matokeo hayo pamoja na ufafanuzi.”
Kwa nyakati tofauti gazeti hili lilimtafuta Dk Kawambwa na Naibu wake, Phillip Mulugo ili kutolea ufafanuzi suala hilo, lakini simu zao za mkononi zilikuwa zikiita bila majibu.
 
 
Msimamo wa Tamongsco
Alipotafutwa Katibu Mkuu wa Tamongsco, Benjamin Nkonya kueleza kama wanakubaliana na agizo hilo la Serikali alisema, “Inaonekana Serikali haiko tayari kutekeleza mkakati wake wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN).”
 
“Kama wizara inalazimisha wanafunzi walio na ufaulu mdogo kuendelea na masomo katika mfumo wa vidato (formal education), lazima tutegemee kuona wanafunzi wakifanya vibaya katika mitihani ya kidato cha nne.”
 
Alisema kuwa asilimia 98 ya wanachama wa chama hicho ni Watanzania wazalendo kwamba hawapo tayari kutekeleza agizo la Serikali kwa sababu siyo la kizalendo na limetolewa kwa ajili ya kutimiza malengo ya kisiasa ya kujiongezea umaarufu wa muda mfupi, huku Watanzania wakiogelea kwenye dimbwi la umaskini unaotokana na ujinga.
 
“Wachache watakaosaliti msimamo huu watakuwa wamekubali kupoteza muda wa vijana wetu huku wakijua kwamba watafika kidato cha nne, kupata daraja sifuri na kuishia kuwa machangudoa, wauza dawa za kulevya, bangi, wizi na vitendo vingine vya uvunjifu wa sheria, kanuni na taratibu,” alisema.
Alisema ili kuwasaidia wanafunzi wanaoshindwa kuendelea na masomo yao; “Mwanafunzi ambaye ufaulu wake utakuwa chini ya asilimia 45 aondolewe katika mfumo wa elimu ya vidato (formal education) na kuingizwa katika mfumo wa elimu ya ufundi mchundo (TVET - Technical education and vocational education).”
 
Alisema wanachama wa Tamongsco wanamiliki vyuo 586 kati ya vyuo 750 vya ufundi mchundo (VETA) nawanamiliki vyuo 1975 kati ya vyuo 1988 vya ufundi stadi (technical institutes) ambavyo vinasimamiwa na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi Stadi (NACTE).
“Vyuo hivi vina uwezo wa kuchukua wanafunzi wote ambao wana ufaulu wa chini ya asilimia 45 kuwaendeleza hadi chuo kikuu. Kikwazo pekee kilichopo ni kwa Serikali kukubali kuchangia gharama za uendeshaji wake.”
 
“Kikwazo hiki kitaondoka endapo Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi itakubali kutekeleza sera, sheria na kanuni za ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi (PPP) partnership) kama ilivyopitishwa na Bunge mwaka 2010.
 
Kidato cha pili 2012
Katika mtihani huo mwaka 2012 wanafunzi 136,923 kati ya 386,271 waliofanya mtihani huo walifeli. Idadi ya waliofeli ilikuwa sawa na asilimia 35.5, wakiwamo wasichana 74,020 na wavulana 62,903, waliofaulu walikuwa wanafunzi 245.9,32.
 
Via: MCL

MABADILIKO YA BARAZA LA MAWAZIRI, MDOGO WAKE MGIMWA, MWIGULU WAULA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
 
 
UHAMISHO NA UTEUZI WA MAWAZIRI NA NAIBU MAWAZIRI
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, amewahamisha na kuwateua baadhi ya Mawaziri na Naibu Mawaziri kama ifuatavyo:-
 
1.0 OFISI YA RAIS
Hakuna mabadiliko.
 
2.0 OFISI YA MAKAMU WA RAIS
2.1 Waziri wa Nchi (Muungano) - Hakuna mabadiliko
2.2 Mhe. Eng. Dr. Binilith Satano MAHENGE (Mb)
Waziri wa Nchi (Mazingira).

 2.3 Mhe. Ummy Ali MWALIMU (Mb)
Naibu Waziri
 
3.0 OFISI YA WAZIRI MKUU
Hakuna mabadiliko
 
 
4.0 WIZARA
 
4.1 WIZARA YA FEDHA
4.1.1 Mhe. Saada Mkuya SALUM (Mb)
Waziri wa Fedha
Mhe. Mwigulu Lameck NCHEMBA (Mb)
Naibu Waziri wa Fedha
4.1.2 Mhe. Adam Kighoma Ali MALIMA (Mb)
Naibu Waziri wa Fedha

4.2 WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA
Hakuna mabadiliko
 
4.3 WIZARA YA KATIBA NA SHERIA
4.3.1 Mhe. Dkt. Asha-Rose Mtengeti MIGIRO (Mb)
Waziri wa Katiba na Sheria
4.3.2 Naibu Waziri - Hakuna mabadiliko

4.4 WIZARA YA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI
Hakuna mabadiliko

4.5 WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA
4.5.1 Waziri - Hakuna mabadiliko
4.5.2 Mhe. Janet Zebedayo MBENE (Mb)
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara
 
4.6 WIZARA YA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA
Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi (Mb)
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

4.7 WIZARA YA UJENZI
Hakuna mabadiliko
 
4.8 WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
4.8.1 Mhe. Mathias Meinrad CHIKAWE (Mb)
Waziri wa Mambo ya Ndani
4.8.2 Naibu Waziri - Hakuna Mabadiliko
 
4.9 WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII
4.9.1 Mhe. Dkt. Seif Seleman RASHIDI (Mb)
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii
4.9.2 Mhe. Dkt. Kebwe Stephen KEBWE (Mb)
Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii

4.10 WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
4.10.1 Waziri: Hakuna mabadiliko
4.10.2 Mhe. Jenista Joakim MHAGAMA (Mb)
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi

14.11 WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO
14.11.1 Waziri: Hakuna mabadiliko
14. 11.2 Mhe. Dkt. Pindi Hazara CHANA (Mb)
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
 
14.12 WIZARA YA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI
14.12.1 Mhe. Dkt. Titus Mlengeya Dismas KAMANI (Mb)
Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
14.12.2 Mhe. Kaika Saning’o TELELE (Mb)
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi

14.13 WIZARA YA KAZI NA AJIRA
Hakuna mabadiliko

14.14 WIZARA YA MAWASILIANO, SAYANSI NA TEKNOLOJIA
Hakuna mabadiliko

14.15 WIZARA YA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI
14.15.1 Waziri - Hakuna mabadiliko
14.15.2 Mhe. George Boniface Taguluvala SIMBACHAWENE (Mb)
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

14.16 WIZARA YA MAJI
14.16.1 Waziri - Hakuna mabadiliko
14.16.2 Mhe. Amos Gabriel MAKALLA (Mb)
Naibu Waziri wa Maji

14.17 WIZARA YA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA
14.17.1 Waziri - Hakuna mabadiliko
14.17.2 Mhe. Godfrey Weston ZAMBI (Mb)
Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika

4.18 WIZARA YA UCHUKUZI
Hakuna mabadiliko

4.19 WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO
4.19.1 Waziri - Hakuna mabadiliko
4.19.2 Mhe. Juma Selemani NKAMIA (Mb)
Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
 
4.20 WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
4.20.1 Mhe. Lazaro Samuel NYALANDU (Mb)
Waziri wa Maliasili na Utalii
4.20.2 Mhe. Mahmoud Hassan MGIMWA (Mb)
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii

4.21 WIZARA YA NISHATI NA MADINI
4.21.1 Waziri - Hakuna mabadiliko
4.21.2 Naibu Waziri (Madini) - Hakuna mabadiliko
4.21.3 Mhe. Charles Muhangwa KITWANGA (Mb)
Naibu Waziri (Nishati)

Balozi Ombeni Y. Sefue
KATIBU MKUU KIONGOZI
Ikulu
DAR ES SALAAM
19 Januari, 2014
 
Ukiangalia baraza hilo jipya, Sura mpya ni:- Mwigulu Nchemba, Stephen Kebwe, Pindi Chana, Zambi, Juma Nkamia, Kaika Telele, Jenister Mhagama, Mahmoud Mgimwa na Dr. Migiro

Wednesday, January 15, 2014

MWALIMU WILAYANI MANYONI AKUTWA AMEJINYONGA CHUMBANI KWAKE

Na. Furaha Venance-Manyoni
 
Mwalimu mmoja wa Shule ya Sekondari Mwanzi iliyoko wilayani Manyoni mkoa wa Singida, amekutwa amefariki kwa kujinyonga. Mwalimu huyo aliyetambulika kwa jina la Godfrey Mtani (33) pichani juu, amekutwa amejinyonga chumbani kwake kwenye nyumba aliyopanga maeneo ya Sayuni huku sababu hasa za kujinyonga kwake zikiwa hazijafahamika wazi.
 
Godfrey Mtani enzi za uhai wake
 
Mmoja wa wapangaji mwenzake ambaye hakutaka kutaja jina lake, alidai kuwa, Mtani, alisafiri kwenda Dodoma ingawa hakujua alienda kwa tatizo gani na alirejea hapo kwake majira ya jioni siku ya jumapili ya tarehe 12/01/2014, lakini wao walishangaa kuona tangu aingie ndani siku hiyo ya jumapili hadi leo [jumatano] asubuhi hawajamuona akitoka nje huku wakisikia redio ikilia na kuna muda simu yake ilikuwa ikiita bila kupokelewa ndipo wakaingiwa na wasiwasi.
 
                                                 Afisa elimu Sekondari mwenye shati jeupe
akiteta jambo na maafisa wenzake
 
"Kwakuwa suala la Mtani kujifungia ndani muda mrefu si mara ya kwanza, lakini kwa hili tuliona ni muda mrefu sana, we fikiria tangu jumapili mpaka leo jumatano mtu yuko ndani tu!" Alisema.
 
HATUA WALIYOCHUKUA WAPANGAJI
Baada ya kuona hali hiyo, wapangaji wenzake wakaamua kwenda kutoa taarifa kazini kwake maana ni jirani na mahali nyumba yao ilipo ili kumtafuta mwalimu ambaye walidhani yuko karibu naye kumjulisha hali hiyo, anasema, "Baada ya wale wenzetu kwenda kutoa taarifa, walirejea na kutujulisha kuwa wametoa taarifa kwa mwalimu mwenzake, baada ya muda kidogo tuliwaona walimu wawili wakiingia na kuelekea moja kwa moja hadi chumba cha marehemu wakiongozana na kijana mmoja wa hapa hapa nyumbani.
Baadhi ya wananchi wakiwa eneo la tukio
 
ILIKUWAJE WALIPOTOKA NDANI?
"Tuliwaona walimu wale wakitoka huku wakiwa kama watu waliochanganyikiwa hivi, tukawauliza vipi? wakatujibu amejinyonga, ujue tulishangaa sana?" akaendelea, "Basi wakawa kama wanashauriana jambo fulani baada ya hapo wakaondoka na kama nusu saa hivi wakawa wamekuja karibia walimu wote wa Shule aliyokuwa akifundisha."
 
KATIKA ENEO LA TUKIO
Watu wa maeneo jirani walikuwa wamekusanyika kila mmoja akitaka kushuhudia kilichotokea, baadaye wakawasili Maafisa Elimu Sekondari na Msingi wilaya wakiambatana na Mkaguzi Kanda [Manyoni], 
 
Mwili huo ulichukuliwa na Polisi na kupelekwa kuhifadhiwa katika hospitali ya Wilaya ya Manyoni kwa  uchunguzi zaidi, juhudi za kumpata OCD kuzungumzia tukio hilo ziligonga mwamba baada ya kuambiwa kuwa alikuwa katika kikao.
 
Taarifa zaidi zinasema kuwa, mwili wa marehemu unaweza kusafirishwa kesho alhamisi mkoani Mara wilayani Serengeti baada ya shughuli za kuuaga mwili wa marehemu katika shule ya Sekondari Mwanzi kukamilika.
 
Marehemu Godfrey Mtani alizawaliwa tarehe 11/04/1980 na mwaka 2011 alihitimu shahada yake ya kwanza katika Chuo cha Elimu (DUCE) na mwaka 2012 mwezi wa pili ndiyo aliajiriwa katika Wilaya hiyo ya Manyoni na kupangiwa Shule ya Sekondari Mwanzi.

Sunday, January 12, 2014

WAKATI STEVEN WASIRA AKIITABIRIA KIFO CHADEMA, MWANAE MWINGINE AJIUNGA CHADEMA

MAGAMBO Wassira ambaye ni mtoto wa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Mahusiano na Utaratibu, Steven Wassira, amejiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
 
 
Akizungumza na Tanzania Daima jana, Magambo alisema hawezi kumfuata baba yake kujiunga na CCM, kwani hayo ni maono yake mwenyewe.
 
 
Magambo ambaye pia ni mgombea wa udiwani katika Kata ya Nyasura, wilayani Bunda, alisema anamuheshimu Wassira kwani ni baba yake mkubwa, lakini hawezi kumfuata kiitikadi.
 
 
Alisema haki pekee inapatikana kwa CHADEMA na kueleza kuwa akishinda amejipanga kuhakikisha uchaguzi mkuu wa mwakani Jimbo la Bunda linapata mbunge wa CHADEMA.
“Mambo ya kifamilia ni ya kifamilia, baba Wassira yeye ameona awe CCM, lakini mtazamo wangu na wake ni tofauti, mimi naona CCM hainitendei haki.
 
 
“Suluhisho la Watanzania ni CHADEMA pekee na ukombozi wa kweli utapatikana kupitia chama hicho kwani si kandamizi,” alisema Magambo.
Uchaguzi mdogo wa madiwani unatarajiwa kufanyika Februari 9 katika kata 27 nchini

Via: Tanzania Daima

MBUNGE WA MOSHI VIJIJINI, MH. CYRIL CHAMI BAADA YA KU AWAITA WENZAKE WANAOSHABIKIA MGOGORO WA CHADEMA SAWA NA MALAYA, LEO ADAI KUWA KINACHOENDELEA NDANI YA CCM NI BALAA KULIKO HILI LINALOENDELEA NDANI YA CHADEMA, UNAJUA NI NINI KINACHOENDELEA CCM? SOMA HAPA

Mbunge wa Moshi Vijijini Mh. Cyril Chami, ambaye pia aliwahi kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara katika serikali hii ya awamu ya nne kuwafananisha wanachama wenzake wa CCM wanaoshabikia mgogoro uliopo ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo [CHADEMA] sawa na Malaya kupitia ukurasa wake wa facebook siku ya ijumaa, leo akiendelea na kuuangazia mgogoro ndani ya cha hicho na kile kinachoendelea ndani ndani ya chama chake CCM, post zote hizi hapa chini:
Cyril ChamiCyril Chami
.... Hii tabia ya wana CCM wenzangu kushangilia wazi wazi mgogoro tata unaoendelea kati ya Mhe. Zitto Kabwe na CHADEMA sijaupenda na wala hauna maana ktk maendeleo ya demokrasia nchini. Maana ya kuwa kwenye mfumo wa vyama vingi ni pamoja na kutokuwa mwanachama wa vyama vingi... Wanachama wa CCM wanaoshabikia suala hili nawaita (Kwa jina baya) kuwa ni sawa na Malaya wa kisiasa.
                                           Nawaomba radhi kwa kutumia maneno makali kwa leo.

Leo ameandika tena hivi:
 
 
 
 
 
.....................Kinachoendelea ndani ya chama changu (CCM) Juu ya Urais 2015 ni hatari kubwa kuliko kinachoendelea CHADEMA na MheZitto Kabwe. Wana CCM tuwe makini.

Saturday, January 11, 2014

HUU NDO WASIFU WA ARIEL SHARON

Ariel Sharon alikuwa mtu asiyejali,mwenye aina ya ukaidi,asiyejali nani anayempenda wala anayemchukia iwe ni Waisrael au Waarabu.

Malengo ya kwanza ya mwanajeshi huyu mstaafu na veterani wa siasa ilikuwa ni kuhakikisha kwanza usalama wa Israel kwa vile alivyoamini.
Sharon hakujali chochote kwa wale wasioamini.
Ndio maana alihakikisha ardhi kubwa na haki ya kisiasa inasalia kwa Waisrael na kutoa nafasi ndogo kwa Wapelestina.
Bwana Sharon alizaliwa nchini Palestina mwaka 1928,ilipokuwa chini ya utawala wa Kiingereza.
Akiwa kijana mdogo alijiunga na kitengo cha jeshi la chini kwa chini la Wayahudi la Haganah na kupigana katika vita vya Israel na Waarabu mwaka 1948-49 baada ya kuundwa kwa taifa la Wayahudi.
Kwenye miaka ya 1950 aliongoza oparesheni kali ya kijeshi dhidi ya kituo cha jeshi la Misri kilichopo kwenye ukanda wa Gaza,katika tukio moja la mwaka 1955 wanajeshi wa misri 38 waliuwawa.
Bwana Sharon alipanda kicheo kutoka brigedia hadi jenerali na kamanda wa kikosi cha jeshi kwenye vita vya siku sita vya mwezi Juni mwaka 1967 ambapo Israel iliuteka ukanda wa Mashariki wa mji wa Jerusalem,Ukindo wa Magharibi na ukanda wa Gaza.

Uny'ang'anyi huo wa nguvu uliofanywa na jeshi la Wayahudi ilizidisha chuki ya Wapalestina kwa mtu ambaye alikuwa adui yao mkubwa.

Alichaguliwa kwa mara ya kwanza kwenye bunge la Israel lijulikanalo kama Knesset mwaka 1973,lakini akajiuzulu mwaka mmoja baadaye ili kutumikia nafasi kama mshauri wa usalama wa aliyekuwa waziri mkuu wa tano wa taifa la Israel bwana Yitzhak Rabin.
Alichaguliwa tena kwenye bunge la Israel mwaka 1977.
Bwana Sharon alikuwa kinara wa uvamizi wa Israel nchini Lebanon mwaka 1982.
Akiwa kama waziri wa ulinzi na bila kumueleza Waziri Mkuu Menachem Begin alituma vikosi vya jeshi la Israel kwenda mjini Beirut,uvamizi ambao ulimaliza na kufukuza chama cha ukombozi cha Palestina kilichokuwa kikiongozwa na Yasser Arafat cha Palestine Liberation Organisation (PLO) kutoka nchini Lebanon.
Uvamizi huo ulisimamisha mashambulizi yaliyokuwa yakifanywa na PLO kupitia nchini Lebanon kuipiga Israel na pia ilisababisha uteswaji mkubwa wa mamia ya Wapelestina kutoka kwa wapiganaji wakristo kutoka Lebaanon chini ya amri ya wanajeshi wa kiyahudi kwenye kambi ya wakimbizi.
Bwana Sharon aliondolewa madarakani mwaka 1983 na mahakama ya Israel ya uchunguzi ya uvamizi wa mwaka 1982 nchini Lebanon, ambapo ilimkuta na makosa kutohusika moja kwa moja na mauaji.
Kwa wanasiasa wengi na wale waliokuwa na mtazamo kama wake huo ndio ulikuwa mwisho wake wa kisiasa.
Lakini kwa bwana Sharon alisalia kiongozi maarufu wa Wayahudi wenye mrengo wa kulia na kuwa imani kwamba muda ungalipo na nafasi nyingine itajitokeza tu.
Ariel Sharon malengo yake ambayo maadui zake waliyaita ya hatari na yenye kukandamiza, ilikuwa ni kupigania hali ya usalama wa ulinzi wa Israel, alimini daima kwamba mwisho hilo lingekuwa suluhisho la haki.
Akiwa waziri wa nyumba kwenye miaka ya 1990,alisimamia na kuongoza ujenzi mkubwa majengo ya wayahudi kwenye Ukingo wa Magharibi na Ukanda wa Gaza tangu Israel iyachukue maeneo hayo kwenye vita vya siku sita.
Baada ya Chama chenye mrengo wa kulia cha Benjamini Netanyahu kuchukua madaraka mwaka 1996, Waziri mkuu mpya wa Israel alitia chagizo kumweka jenerali huyo wa zamani wa jeshi kwenye baraza lake la mawaziri.
Wakati alipomchagua kama Waziri wa mambo ya nje mwaka 1998, Bwana Netanyahu alisema Ariel Sharon alikuwa mtu sahihi kwa nafasi hiyo.
Meja Jenerali wa jeshi la Israel, Ariel Sharon(aliyeko kushoto mbele) akiwa ndani ya gari ya kijeshi aina ya Jeep mwezi October mwaka 1973. Picha na Wizara ya Ulinzi ya Israel.

" Hatutakiwi kufikiria yaliyopita" alisema. " ana rekodi katika maisha yake yote ya kutumikia uma na katika miaka 15 iliyopita watu wanatakiwa kujivunia naye."

Bwana Sharon alichaguliwa kuwa kiongozi wa chama wa mrengo wa kulia cha Likud kilichokuja kuwa chama cha Upinzani baada ya anguko kubwa la Netanyahu kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 1999.
Baada ya kushindikana kwa mapatano kwenye mkutano wa amani ya Palestina na Israel ujulikanao kama Camp David mwaka 2001,bwana Sharon alipigania tena kurejea kwenye ofisi za uma akimpinga waziri mkuu wa wakati huo Ehud Barak,huku akimtuhumu kwa kuwa tayari kuiuza Jerusalem kwaajili ya mapatano ya amani.

" Barak hana haki ya kukata tamaa juu ya Jerusalem,ambayo watu walipokea kama urithi," Bwana Sharon alisema kwenye mojawapo ya vikao vya bunge.

Ziara yake yenye utata mwaka 2000 kwenye msikiti wa Al Aqsa mashariki mwa Jerusalem, eneo ambalo pia ni eneo takatifu kwa Wayahudi,ilikuwa ni kutonesha kidonda kwa mara ya pili kwa kuamsha vuguvugu la Wapelestina.
Wasioamini wanasema bwana Sharon alijuwa fika kuwa ziara yake hiyo ingeleta vurugu na alifanya hivyo kwa makusudi ili kuwaonyesha Wayahudi kuwa kiongozi kama yeye ndiye atakayeweza kumudu hali hiyo.
Lakini kwa mara nyingine tena, bwana Sharon hakuwahi kusikia wala hakujali wasioamini walimweleza nini.
Katika nyakati fulani kwenye mikutano ya kampeni za uchaguzi mkuu aliwahi kusema anajiandaa kufanya mazungumzo na kuingia makubaliano ya amani na Waarabu lakini sio chini ya vitisho.
Licha ya yote alikuwa tayari kufanya lolote ili kuondoa hali ya uonevu utakao ondoa "haki ya Wayahudi kuishi kwa amani kwenye ardhi yao"
Ariel Sharon malengo yake ambayo maadui zake waliyaita ya hatari na yenye kukandamiza, ilikuwa ni kupigania hali ya usalama wa ulinzi wa Israel, alimini daima kwamba mwisho hilo lingekuwa suluhisho la haki.
 
Via BBC Swahili

SUGU ENZI HIZO 1996 LIVE PERFORMANCE, SONG, NI WAPI TUNAKWENDA,

 
Katika kitabu chake Sugu, alichokipa jina la 'MUZIKI NA MAISHA' ukurasa wa 58 na 59 amezungua Show aliyoifanya Mnazi Mmoja jijini DSM, baada ya kuunganishwa na John Kitime, Sugu mwenyewe anazungumzia aliipania sana hiyo show, anaendelea kusema kuwa, "Waliokuwa wakiubeza muziki huu walipigwa na butwaa zaidi, Tanzania nzima ilishuhudia mlipuko ule kupitia ITV, tena Watanzania wa tabaka zote..."
 
 
Sasa tumekuletea show yenyewe, tunaamini wale tulioanza kufuatilia mziki huu tangu enzi hizo tutakuwa tumekumbuka mbali sana, Mzigo wenyewe huu hapa chini, icheck video hii mtu wangu.

Thursday, January 2, 2014

HIZI NDIZO AGENDA ZA KIKAO CHA KAMATI KUU CHADEMA KESHO

Kutokana na maswali kutoka kwa wanahabari wa vyumba mbalimbali vya habari juu ya agenda za kikao cha Kamati Kuu kesho, Chama kimetoa kauli ifuatayo;
 
Ni kweli kutakuwa na mkutano maalum wa Kamati Kuu ya chama kesho tarehe 3 Januari 2014 Jijini Dar Es Salaam. Ajenda kuu katika mkutano huo ni tatu;
 
Mosi; Kupokea taarifa kuhusu mchakato na maudhui ya mabadiliko ya katiba
 
...
Kamati Kuu itapokea taarifa juu ya kupitishwa kwa marekebisho ya sheria ya mabadiliko ya katiba 2013, kupitishwa kwa muswada wa kura ya maoni wa 2013, uteuzi wa wajumbe wa Bunge Maalum na kutolewa kwa Rasimu ya Katiba Mpya.
 
Pili; Kupokea utetezi (wa mdomo) wa wanachama watatu kuhusu tuhuma mbalimbali zilizoelekezwa kwao.
 
Wanachama hao walishajulishwa makosa yao kwa maandishi na wamewasilisha utetezi wao wa maandishi. Wataitwa kwenye kikao kwa kuzingatia matakwa ya kanuni 6.5.2 (b) na 6.5.2 (d) kupewa nafasi ya kujitetea mbele ya kikao kinachohusika.
 
Tatu; Mpango Kazi wa Chama kwa mwaka 2014
Mpango Kazi wa chama ni sehemu ya hatua za utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Chama wenye dhima ya kuleta uongozi bora, sera sahihi, mikakati makini na oganizesheni thabiti kwa maendeleo endelevu ya chama na taifa.

John Mnyika
Mkurugenzi wa Mawasiliano

Wednesday, January 1, 2014