Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Friday, June 23, 2017

HAWA NDIO WALIOTETEA UCHOTWAJI FEDHA ZA ESCROW

WALIOTETEA UCHOTWAJI FEDHA
Pamoja na Kamati ya PAC kuwasilisha ripoti yake juu ya suala hilo ambapo ilijiridhisha kuwa sehemu ya fedha hizo ni za Serikali, baadhi ya wabunge na mawaziri walipinga hatua hiyo na kusema kuwa fedha hizo hazikuwa za umma bali ni mali za IPTL.
Mmoja wa mawaziri waliosimama bungeni kutetea suala hilo ni aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ambaye alizungumza kwa kujiamini kuwa fedha hizo si mali ya umma.

 LUSINDE
Tokeo la picha la lusinde livingstoneMbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde (CCM), akichangia ripoti hiyo ya PAC bungeni, alisema hata Zitto ambaye ni mwenyekiti wa kamati alipokea fedha kutoka kwa Sethi.
“Zitto ni rafiki yangu mkubwa na aliwahi kunisaidia nilipokuwa na tatizo, lakini katika hili lazima niseme kwamba ulipokea fedha kutoka kwa Sethi, atupe jibu isije kuwa tunakaa hapa kumbe walaji wako wengi. Kwa nini Tibaijuka anapopewa inakuwa fedha haramu, lakini kwa Zitto ni halali?
“Na Zitto anahusika, Kafulila naye anakuja hapa ohh eti taarifa ya siri imevuja tujadili, tujadili kwani ninyi Mungu?” alihoji Lusinde.

 MOHAMED CHOMBO
Mbunge wa Magomeni, Zanzibar, Mohamed Chombo (CCM) alisema: “Nimesikiliza ripoti ya PAC na Serikali, lakini jambo hili lipo wazi kwamba hizi fedha hazikuwa za umma, zilikuwa za IPTL zimelipwa na Tanesco.”

RICHARD NDASA
Tokeo la picha la RICHARD NDASA
Mbunge wa Sumve, Richard Ndassa (CCM), alisema kumezuka mtindo wa kusingiziana na kwamba wabunge wa aina wamwogope Mungu.
“Tusiwavunje moyo wizara, wamefanya kazi kubwa, tushauri pale kwenye tatizo tuseme sasa fukuza huyu halafu nini kinafuata?
“Tukiwa na utaratibu wa kufukuzana itaendelea hivyo hivyo, tumwogope Mungu, lakini nafsi zetu zitatusuta kwa sababu ya matendo yetu. Hivi sasa kamezuka mtindo wa kusingizia mtu huyu kala, huyu kapewa mtu akipewa asimame hapa aseme amepewa, lakini tusiwasingizie,” alisema Ndassa.


 MARIAM KISANGI
Mbunge wa Viti Maalumu, Mariam Kisangi (CCM), alisema upinzani baada ya kuona kwamba chama tawala kinapeta wakaamua kuwakoroga na Escrow.
“Tuangalie utendaji wa watu na ninawaambia hatoki Muhongo wala Maswi, CCM kitapita na hiyo ndiyo njama zenu upinzani kutukoroga. Mmekaa mkao na CCM inapeta, mkajisemea hawa tuwakoroge na nini ndio mkaja na Escrow mara EPA, nawaambia njama zenu hazisaidii.
“Zile fedha si za umma. Tanesco ina madeni mengi, inadaiwa Sh bilioni 700. Waziri ameeleza vizuri, kwa hiyo tusipotezeane muda hapa,” alisema mbunge huyo. 

SIMBACHAWENE
Tokeo la picha la simbachawene 
Aliyekuwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini na Mbunge wa Kibakwe, George Simbachawene, naye alitumia mbinu zote kutetea ufisadi huo na wakati mwingine alijenga hoja ili watuhumiwa waweze kupenya.

No comments:

Post a Comment