Katika ukurasa wake wa facebook Dk. Kitila ameandika haya kuhusu nafasi za Ukuu wa Wilaya:

Ndiyo maana vyama vyote makini vya upinzani vimeweka katika ilani zao kufuta nafasi ya ukuu wa wilaya kama sera muhimu ya kubana matumizi na kuzipa mamlaka kamili halmashauri zetu zifanye kazi ya kuwaletea wananchi maendeleo. Siku nikipata nafasi ya kumsogelea mheshimiwa Rais nitamnong’oneza jinsi ambavyo kufuta nafasi ya ukuu wa wilaya ingemrahisishia kazi ya kuwahudumia maskini kama alivyopania. Njia rahisi ya kudhihirisha azma na nia ya kubana matumizi kwa Rais wetu ni kutumia mamlaka yake kikatiba kufuta hii nafasi ya ukuu wa wilaya haraka. Hii ni muhimu zaidi kuliko kufuta/kuahirisha sherehe za Uhuru na Muungano ambazo ndio alama kuu ya Taifa letu tulipendalo. Watanzania wenzangu tumuombee sana Mheshimiwa Rais wetu ili Mungu amfungulie aione busara ya kufuta hii nafasi ya ukuu wa wilaya katika mfumo wetu wa utawala. Hayo ndiyo maoni yangu.
No comments:
Post a Comment