Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Friday, October 24, 2014

MAELFU WAMZIKA FR. MAKWANDA, ATHIBITISHA KUWA ALIKUWA KIPENZI CHA WATU, MKUU WA MKOA SINGIDA AMPA TANO.


Na.Venance Furaha-Manyoni

Wakazi wa Manyoni na vitongoji vyake na wageni mbalimbali kutoka Mkoa wa Singida na mikoa mingine nchini wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Singida Ndugu Parseko Kone, wamejitkeza kwa wingi leo kumzika Fr. Makwanda aliyefariki kwa ajali ya gari wakati akitokea Itigi kwenda Manyoni. ajali hiyo iliyotoa uhai wa Fr. Makwanda ilitokea eneo la Mabondeni usiku wa jumatatu, tarehe 20/10/2014. ajali hiyo huenda ilitokea kati ya Saa nne au tano usiku hivi. Mji mzima wa Manyoni ni kama ulikumbwa na simanzi baada ya taarifa za kifo cha Padri huyo kuanza kusambaa. Baadhi ya wakazi wa Manyoni wakiongea na BabaD Blog.wakimuelezea Padri huyo, walisema kuwa   alikuwa mtu mcheshi, mkarimu, na aliyependa kujichanganya na kila mtu bila kujali dini ya mtu.
"Kusema kweli ndugu yangu huu msiba ni pigo kubwa sana si kwa Wakatoliki pekee bali kila mtu aliyekuwa akimfahamu huyu jamaa atakuwa ameguswa na tukio hili" Alisema Mzee Juma aliyejitambulisha kuwa anatokea maeneo ya Majengo. 

Mkazi mwingine wa Manyoni ambaye hakutaka kujitambulisha jina lake, alidai kuwa Padri Makwanda ni kama alijitabiria kifo, "Ujue padri wetu ni kama alikuwa anajua kuwa hivi karibuni hatakuwa nasi, ni juzi juzi tu alikuwa anatuonesha  eneo ambalo kama akitangulia kufa mwili wake utapumzishwa na hapo na ndipo alipopumzishwa siku ya leo (Jana) kweli huyu  padri alikuwa kipenzi cha watu ona umati wote huu!"

Akimzungumzia marehemu, Mkuu wa Mkoa wa Singida Bw. Parseko Kone, alisema kuwa Fr. Makwanda alikuwa mtu wa watu, mara nyingi nikiwa hapa manyoni Fr. Padri Makwanda alinipa sehemu ya kulala, alinihudumia chakula hakika nilikuwa nahudumiwa kama mtoto...katika hali ya kibanadamu Fr. Makwanda alikuwa kama kijana wangu, lakini kiroho alikuwa ni baba yangu." Alisema Mkuu wa Mkoa.

Wageni wengine waliohudhuria ni pamoja na Mkuu wa wilaya ya Manyoni Bi. Fatuma Tawafiq, vingozi mbalimbali wa dini kutoka madhehebu na dini mbalimbali, wawakilishi mbalimbali kutoka Parokia na majimbo mbalimbali.

Mwili wa marehemu kabla ya kupumzishwa katika nyumba yake ya milele, misa ya kumuombea marehemu  ilifanyika katika kanisa la RC Manyoni, Parokia ya Kupaa Bwana na baada ya shughuli ya kuuaga mwili wa marehemu yalifuatiwa na maandamano kuelekea makazi ya Mapadri ambako ndiko Mwili wa Fr. Makwanda ulipolazwa.

Mpaka mauti inamkuta Padri Makwanda alikuwa ni Msaidizi wa Paroko parokia ya Kupaa Bwana Manyoni.

BWANA AMETOA BWANA AMETWAA, JINA LA BWANA LIHIMIDIWE

Fr. Makwanda enzi za uhai wake


Fr. Makwanda enzi za uhai wake

Jinsi ilivyokuwa maeneo ya makaburini
















Hii ndiyo gari aliyopata nayo ajali

Baba D. blog inaungana na Wanamanyoni wote kuipa pole familia ya Fr. Makwanda, Paroko wa Parokia ya Kupaa Bwana na waumini wote wa parokia hiyo. R.I.P Fr. Makwanda.

Picha kwa hisani ya Sylvery Hussein, Edga Madeje na wadau wengine.

No comments:

Post a Comment