Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Sunday, August 25, 2013

SAKATA LA MADAWA YA KULEVYA, MBUNGE WA NZEGA, Dr. KIGWANGALLA AJITOA MHANGA KUWATAJA WAHUSIKA

Hamisi KigwangallaSakata la madawa ya kulevya limechukua sura mpya, baada ya mbunge wa Nzega Hamisi Kigwangalla kuahidi kuwaanika wote wanaojihusisha na biashara hiyo haramu, akitumia ukurasa wake wa facebook Mh. Kigwangalla ameandika kuwa, kupitia Bunge lijalo, atajitoa mhanga kuwaanika wote, hivyo na kuwataka wananchi wanaowajua wauza  'unga' wampe ushirikiano kwa kumpenyezea majina ya wahusika. kupitia ukurasa wake huo, ameandika hivi:
 
 
 "Kuna watu wengi sana mtaani wanadai wanawajua wauza dawa za kulevya. Mimi najitoa mhanga kuwaanika hadharani kupitia Bunge litakaloanza keshokutwa. Naomba sasa kila mwenye taarifa sahihi kuhusu mtu yeyote anayefahamika kujihusisha na biashara ya madawa ya kulevya anipenyezee ili mimi nimfunge paka Kengele. Tuache siasa na minong'ono isiyo na tija, leteni taarifa tuchukue hatua!"

No comments:

Post a Comment