Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Sunday, November 4, 2012

CHILIGATI AWAONYA WANAOTAKA MUUNGANO UVUNJWE


Asema:  Kama muungano ungekuwa ni sumu inayojaribiwa, tungethubutu kuuvunja kwa muda kidogo...
 
 
 
Katika kuchangia maoni yake kwa tume ya mabadiliko ya katiba. Mh. Chiligati amenukuliwa akisema.; “Kama muungano ungekuwa ni sumu inayojaribiwa, tungethubutu kuuvunja kwa muda kidogo, kule Zanzibar Watanzania elfu 15, na Wanzanzibari walioko bara laki 2.5 waonje adha ya kutafuta hati ya kusafiria au waambiwe wahame, tungejaribu kufanya hivyo.”
Aliendelea kukosoa  mfumo wa serikali tatu ambao baadhi ya wabunge walikuwa wakiupendekeza, Chiligati alisema kuwa, unaongeza gharama kwa sababu utahitaji Baraza la Mawaziri na rais mwingine, na kwamba Tanganyika iliyokufa itabidi ifufuliwe.
 
Maoni hayo ya Mh. Chiligati yametolewa jana ikiwa ni siku tatu kabla ya ukusanyaji wa maoni kwa wakazi wa Manyoni kuanza rasmi siku ya jumanne tar. 06 Nov. Je wanamanyoni tunasemaje? tunataka katiba ijao iweje? basi tujitokeze kwa wingi siku hiyo ili kushiriki kutoa maoni yetu na hivyo kuwa sehemu ya mabadiliko ya Katiba hayo.

No comments:

Post a Comment