Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Sunday, November 4, 2012

Afisa Elimu avuliwa madaraka





BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma, limemvua madaraka ofisa elimu wa shule za sekondari, Bilungama Nyalinga, kutokana na tuhuma zilizokuwa zikimkabili.

Akitoa taarifa ya kuvuliwa madaraka hayo wakati wa kikao cha baraza la madiwani, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Juma Maganga, alisema kuwa uamuzi huo umekuja baada ya tume kufanya uchunguzi wa kina juu ya tuhuma zilizokuwa zikimkabili ofisa huyo.

Maganga alizitaja tuhuma zilizokuwa zikimkabili kuwa ni kutumia vibaya madaraka aliyokuwa nayo, matumizi mabaya ya fedha za ofisi, kuwa na mahusiano mabaya na walimu anaowaongoza, na kushuka kwa kiwango cha elimu wilayani hapo.

“Nyalinga hatakuwa na cheo cha ofisa elimu katika wilaya hii kuanzia sasa, na anaruhusiwa kukata rufaa mahali popote tangu pale atakapokuwa amepokea barua ya kumtaarifu juu ya suala hili,” alisema Maganga.

Alisema kuwa kabla ya kuvuliwa madaraka, alisimamishwa kazi na baraza hilo kwa miezi mitatu iliyopita na kuundwa kwa tume ya uchunguzi iliyokuja na ripoti ya kubaini madudu hayo yaliyokuwa yakimkabili.
 
 
Chanzo: Tanzania Daima Jumapili 04 Nov. 2012

No comments:

Post a Comment