Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Monday, November 5, 2012

RAIS KIKWETE AZINDUA BARABARA YA MANYONI-ISUNA



      Rais akiwahutubia wananchi

Na. Furaha Venance : Manyoni-Singida
 
Ufunguzi wa barabara hiyo ya lami Manyoni – Isuna yenye urefu wa kilometa 54 imezinduliwa leo na rais wa Jamhuru ya Muungano  wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, kabla ya ufunguzi huo, mkuu wa wilaya ya Manyoni mama Fatuma Tawafiq alikaribisha Mkuu wa mkoa Dr. Paseko. Kone kuzungumza na wananchi kidogo na kufanya utambulisho wa wageni walioongozana na msafara wa rais.

 

Ilipowadia nafasi ya Mh. John Chiligati mbunge wa Manyoni Mashariki kuzungumza na wananchi, aliwahakikishia wakazi wa Manyoni kuwa, ujenzi wa barabara ya Manyoni inayoingia mjini kati yenye urefu wa kilometa 4.5 haijasahaulika amekuwa akizungumza na waziri wa ujenzi na kumuahidi kuwa barabara hiyo itajengwa hivyo aliwataka wakazi hao wasiwe na wasiwasi kuhusu barabara hiyo.
 
Mh Chiligati pia aligusia tatizo la maji, ambapo alisema kuwa ili kutatua tatizo la maji, kazi mbili zinatakiwa kufanywa, kwanza ni kujenga tenki lenye uwezo wa kuhifadhi maji lenye ujazo wa lita milioni moja lililopo halikidhi kwa kuwa lina ujazo wa lita laki mbili na nusu tu, ujazo ambao ni mdogo ukilinganisha na mahitaji ya wakazi wa wilaya hiyo, kazi ya pili inayotakiwa kufanywa ni usambazi wa maji kutoka bwawa la Mbwasa na kuyasambaza katika vijiji vya bonde la ufa ambao hukabiliwa na tatizo la maji,


                                                        Chiligati akiongea na wananchi

Kuhusu umeme mbunge huyo alisema kuwa inahitajika kutoa umeme mjini na kupeleka vijijini, aliendelea kufafanua kuwa mradi wa kwanza wa kusambaza umeme wa vijiji kumi, vijiji saba umeme umefika na kuna vijiji vitatu vilisahaulika katika mpango huo ambavyo ni,  Mbwasa, Maweni na Sukamahela ambavyo kwa sasa vijiji hivyo vipo kwenye mpango.

 

Chiligati alimuomba Mh. Rais kuwezesha wakazi wa Nkoko kupata umeme, katika hili alisema, “..Mh. Rais wewe ndiye rais wa kwanza katika nchi hii kufika Nkoko na naomba uwe rais wa kwanza kukipatia kijiji cha Nkoko umeme..”

 

Mwisho Chiligati aliwataka wana Manyoni kuwapuuza wote wanaopita pita wakiwadanganya wananchi kuwa wanaleta mabadiliko, “..kuna watu wanazunguka walienda Morogoro, wakaenda na Iringa na hapa watakuja, ndugu zangu, wakija …ndugu zangu wana Manyoni tushikamane…” Inaelekea hapa alikuwa anakizungumzia Chama cha Demokrasia na Maendeleo [CHADEMA] ingawa hakukitaja chama chenyewe,maana ndiyo kumbukumbu zinaonesha wamepita huko na ile Operesheni yao waliyoibatiza kwa jina la M4C.

 
 
        Mh. Magufuli akiteta jambo na Mh. Chiligati na viongozi wengine

Ulipowadia wasaa wa Waziri wa Ujenzi Mh. John Pombe Magufuli alisema kuwa barabara hiyo ya Manyoni –Isuna ina urefu wa Kilometa 54 na imetengenezwa kwa pesa za ndani kiasi cha Tsh. Bilioni 32,

 

“Ujenzi wa barabara hiyo uliamia hapa ilipojengwa kutoka Manyoni mjini ili kuepuka bomoa bomoa nyumba za watu lakini cha ajabu watu wanaifuata hii barabara, napenda niwambie hao wote walioifuata barabara hii tutawabomolesha, tena ngoja niwaambie kuifuata barabara ni kutafuta umasikini.” Alisema Magufuli.

 

 Kuhusu barabara ya Manyoni mjini kati, Mh. Magaufuli alisema tatizo halipo kwa selikali kujenga barabara hiyo, tatizo lipo kwa Mkandarasi wa Wilaya aliyedizaini ujenzi wa barabara hiyo alileta mapendekezo kuwa ujenzi wa kilomita 1.2 ni bilioni 1.2 kwa kiwango cha lami wakati zipo barabara zimejengwa kwa milioni 250 hadi 300 kwa kilometa na zingine zimejengwa kwa milioni 680 hadi 800  yeye bilioni moja tena barabara ya wilaya!
 
Hivyo Magufuli aliwahakikishia wakazi wa Manyoni Barabara hiyo itajengwa na Mkandarasi wa Wilaya hatakiwa kuiangalia wala kuisogelea barabara hiyo itasimamiwa na Mkandarasi wa Mkoa na kuzitaka Mamlaka husika kumfukuza kazi Mkandarasi huyo au kumshusha cheo akafanye kazi zingine.

 

Rais Jakaya M. Kikwete  aliyotoa ahadi ya kujenga tenki kubwa la maji kupunguza tatizo la maji Manyoni, kuhusu matatizoya maji vijiji vya bonde la ufa , katika atua nyingine Rais aliwapandisha jukwaani Mkurugenzi na Mhandisi wa Maji Wilaya kuwataka kueleza kwanini hawajashusha maji kutoka Mbwasa kwenda vijiji hivyo

Na kuiagiza Halmashauri kuuingiza mradi huo katika mipango yao kama mradi na yeye atawasaidia kuwasemea.

 

Na kuhusu umeme katika kijijicha Nkoko Mh. Rais aliahidi kuwa kijiji hicho kitapata umeme, kuhusu ELIMU serikali itajitahidi kutatua tatizo la vitabu katika shule zake pia aliwaagiza wakuu wa mikoa na wilaya kuhakikisha ndani ya miaka miwili shule zote za kata zinajengwa maabara za sayansi na kuahidi kutatua tatizo la walimu katika wilaya hii katika mgao wa walimu mwaka huu.

 

Vilevile Mh. Rais aliwataka wananchi kujiepusha na ngono zembe ili kuepuka maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi, kuhusu AFYA alisema kuwa serikali yake imefanikiwa kujenga vituo vya afya na zahanati ili kupunguza vifo vya akina mama wakati wa kujifungua, pia wananchi wamepewa vyandarua kujikinga na malaria na kuwataka wananchi wasitumie vyandarua hivyo kufugia kuku au kuvulia samaki.

 

Katika uzinduzi huo viongozi mbalimbali wa kidini kisiasa na serikali walihudhuria, pamoja na hao viongozi wengine waliohudhuria ni pamoja na Wakuu wa wilaya ya Iramba na Singida, Mbunge wa Iramba Mwiguli Nchemba, wabunge wa viti maalumu Diana Chilolo na Martha Mlata, Mwenyekiti mpya wa CCM Mkoa wa Singida Mgana Msindai, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Lazaro Nyarandu, Naibu waziri wa Ujenzi na wengine wengi.

 

Chanzo: mimi mwenyewe

No comments:

Post a Comment