Kitendo cha Askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania [JWTZ] kupiga picha akiwa na makada wa CHADEMA huku akiwa amevaa sare za jeshi hilo [kombati] na akionesha alama ya vidole viwili inayotumia na Chama hicho amezua gumzo katika mitandao ya kijamii na hata miongoni mwa wananchi ambao wameiona picha hiyo katika gazeti la Mwananchi la leo.
Wapo wanaoona kitendo cha wabunge hao kupiga picha na askari huyo huku wakijua kuwa ni kukiuka sheria za nchi ambazo wabunge hao wanazihamu zinazokataza askari yoyote wa majeshi ya Tanzania kuwa mwanachama au kushabikia chama chochote cha siasa ni kitendo kisichofanaa na kinachotakiwa kukemewa na watu wote bila kujali itikadi za vyama vyao. lakini wapo wanaoona kitendo cha askari huyo kujitokeza hadharani na kuonesha mapenzi yake kwa chama chake ni kitendo cha kishujaa na kuonesha kuwa hata askari nao wamechoshwa na chama cha mapinduzi [ccm] kinachotawala kwa sasa.
Nisikuchoshe kwa maelezo mengi angalia picha hizo chini ambazo zimeonekana kutawala na kuibua gumzo katika mitandao mbalimbali ya kijamii na wewe unaweza weka maoni yako baada ya kuangalia picha hizi.
![Hizi ni Mojawapo za Kauli zilizosemwa na Mbunge wa Arusha Mjini @[121554547955586:274:Godbless Lema] jana katika Uwanja wa Mamlaka ya Mji Mdogo Mirerani - Manyara.
→ '' .........Tanzania mna Tanzanite, mna dhahabu, mna Almasi, mbuga za wanyama, mna Milima, mna bandari tano, mna Mafuta, Mna Korosho, Kahawa, mna Pamba, chakushangaza Tanzania Nchi ya Tatu @[0:1:Ombaomba] Duniani.....''
→ ''..........Raaisi mwanaume ombaomba kupita wote Duniani ni Kikwete.........''
→ ''.... .... na sasaivi Kikwete ameanzisha dili nyingine, ya kuchukua @[0:1:Mateja] anawapeleka Ikulu. Hamkumwona akiwa na Teja juzi, Ray C. Alianza na Mamis tukaona inapita, sasa anaanza kuwachukua Mademu Teje anawapeleka Ikulu..
....wewe Kikwete wewe kama Lengo lako ni kusaidia watu waliokula Madawa ya kulevya, Ray C sio peke yake, nenda Mtaani chukua @[0:1:Masela] waliochanganyikiwa kaa nao Ikulu...
→ ''........uwanja wa kia huu, huwezi kupita na TSh 100/= mfukoni..... ...lakini Twiga anapita, Nyati anapita, Usalama wa Taifa uko wapi? Maaskari wako wapi? Mkitaka mkamwambie Kikwete, hautumwogopi Mtu yeyote kuanzia Raisi mpaka Balozi......''
→ ''......mafisadi wa mabilioni ya pesa wanapewa adhabu ya kujiuzulu, mwizi wa simu, TV anapewa adhabu ya @[0:1:kifungo] miaka kumi jela.....''
→ ''......viongozi wa CCM ni wahuni, Ila wamejificha na Suti. Vibaka wa Unga Limited na Vibaka wa Sokoni one, tofauti yao na Mawaziri wa Kikwete na Kikwete mwenyewe ni Mavazi tu, lakini wote ni Wezi.........cha kushangaza mwizi wa billions of Money anapita Mtaani, anapanda Ndege, anapungia watu mitaani, nyie @[0:1:mnachoma] watu mitaani wanaoiba Kuku na Simu.....''](http://sphotos-a.ak.fbcdn.net/hphotos-ak-ash4/s480x480/603339_385394684888957_2118415942_n.jpg)
Godbless Lema akihutubia mkutano wa hadhara huko Mererani
Askari wa JWTZ akiwa mguu pande kumsikiliza Lema na makada wengine wa CHADEMA

Hapa Lema akiwa katika picha na Askari huyo huku akiwa amenyoosha alama ya vema alama inayotumiwa na chama hicho


Kamanda wa JWTZ akiendelea kusikiliza na kufuatilia mkutano
Pia unaweza bofya hapa ~ http://j.mp/Tje9o9
Pia unaweza bofya hapa ~ http://j.mp/Tje9o9
No comments:
Post a Comment