Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Monday, December 24, 2012

MWANAJESHI AZUA BALAA KWA KUPIGA PICHA NA MAKADA WA CHADEMA AKIONESHA ALAMA YA VIDOLE VIWILI HUKU AKIWA NA GWANDA ZA JESHI HILO

Kitendo cha Askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania [JWTZ] kupiga picha akiwa na makada wa CHADEMA huku akiwa amevaa sare za jeshi hilo [kombati] na akionesha alama ya vidole viwili inayotumia na Chama hicho amezua gumzo katika mitandao ya kijamii na hata miongoni mwa wananchi ambao wameiona picha hiyo katika gazeti la Mwananchi la leo.
 
Wapo wanaoona kitendo cha wabunge hao kupiga picha na askari huyo huku wakijua kuwa ni kukiuka sheria za nchi ambazo wabunge hao wanazihamu zinazokataza askari yoyote wa majeshi ya Tanzania kuwa mwanachama au kushabikia chama chochote cha siasa ni kitendo kisichofanaa na kinachotakiwa kukemewa na watu wote bila kujali itikadi za vyama vyao. lakini wapo wanaoona kitendo cha askari huyo kujitokeza hadharani na kuonesha mapenzi yake kwa chama chake ni kitendo cha kishujaa na kuonesha kuwa hata askari nao wamechoshwa na chama cha mapinduzi [ccm] kinachotawala kwa sasa.
 
Nisikuchoshe kwa maelezo mengi angalia picha hizo chini ambazo zimeonekana kutawala na kuibua gumzo katika mitandao mbalimbali  ya kijamii na wewe unaweza weka maoni yako baada ya kuangalia picha hizi.
 
Hizi ni Mojawapo za Kauli zilizosemwa na Mbunge wa Arusha Mjini @[121554547955586:274:Godbless Lema] jana katika Uwanja wa Mamlaka ya Mji Mdogo Mirerani - Manyara.


 →  '' .........Tanzania mna Tanzanite, mna dhahabu, mna Almasi, mbuga za wanyama, mna Milima, mna bandari tano, mna Mafuta, Mna Korosho, Kahawa, mna Pamba, chakushangaza Tanzania Nchi ya Tatu @[0:1:Ombaomba] Duniani.....''


 → ''..........Raaisi mwanaume ombaomba kupita wote Duniani ni Kikwete.........''


 →  ''.... .... na sasaivi Kikwete ameanzisha dili nyingine, ya kuchukua @[0:1:Mateja] anawapeleka Ikulu. Hamkumwona akiwa na Teja juzi, Ray C. Alianza na Mamis tukaona inapita, sasa anaanza kuwachukua Mademu Teje anawapeleka Ikulu..
 ....wewe Kikwete wewe kama Lengo lako ni kusaidia watu waliokula Madawa ya kulevya, Ray C sio peke yake, nenda Mtaani chukua @[0:1:Masela] waliochanganyikiwa kaa nao Ikulu...


 →  ''........uwanja wa kia huu, huwezi kupita na TSh 100/= mfukoni.....   ...lakini Twiga anapita, Nyati anapita, Usalama wa Taifa uko wapi? Maaskari wako wapi? Mkitaka mkamwambie Kikwete, hautumwogopi Mtu yeyote kuanzia Raisi mpaka Balozi......''


 →  ''......mafisadi wa mabilioni ya pesa wanapewa adhabu ya kujiuzulu, mwizi wa simu, TV anapewa adhabu ya @[0:1:kifungo] miaka kumi jela.....''


 →   ''......viongozi wa CCM ni wahuni, Ila wamejificha na Suti. Vibaka wa Unga Limited na Vibaka wa Sokoni one, tofauti yao na Mawaziri wa Kikwete na Kikwete mwenyewe ni Mavazi tu, lakini wote ni Wezi.........cha kushangaza mwizi wa billions of Money anapita Mtaani, anapanda Ndege, anapungia watu mitaani, nyie @[0:1:mnachoma] watu mitaani wanaoiba Kuku na Simu.....''
Godbless Lema akihutubia mkutano wa hadhara huko Mererani
 
Huyu msoja nilikua nae jana kwenye mkutano akaniambia yuko tayari kufutwa kazi na kujiunga na makamanda wa Chadema kwasababu anaipenda Chadema na Awezi kujizuia.
Askari wa JWTZ akiwa mguu pande kumsikiliza Lema na makada wengine wa CHADEMA
 
 
'Mwanajeshi aliyepiga picha na lema tutamfukuza kazi ndani ya saa 24' by Nape Nnauye 

source:wapo radio
Hapa Lema akiwa katika picha na Askari huyo huku akiwa amenyoosha alama ya vema alama inayotumiwa na chama hicho
 
 
Lema, nassari, heche, millya waanzisha jeshi la chadema.

    kwanza nasikitika kwa kuandika habari hizi mimi nilikuwa kwenye huu mkutano jana uliofanyika Mji mdogo wa Mererani uliohudhuriwa na hawa vijana, kuha mwanajeshi alikuwaja kwenye mkutano na kumfuata LEMA na kumpigia saluti, huyu mwanajeshi huwa anafundisha mgambo mjini mererani, jana wakati chadema wakifanya mkutano wa hadhara mwanajeshi huyo aliwaamuru mgambo wote waende kwenye mkutano kuwasikiliza wabunge wa chadema, kabla mwanajeshi huyu haja fikia uwamuzi huo, kuna haice moja ilikuja na makamanda kadhaa wa Chadema, akiwepo mpambe mmoja wa Millya, Oleleshwa alikwenda kuongea na huyu mwanajeshi huyo na ndo migambo wakapewa amri ya kwenda kwenye mkutano, bado niko hapa Mererani nafanya uchunguzi wa kina na nimesha gundua kuwa, Lema, Nassari, Heche wakishirikiana na Millya wanatengeneza Jeshi na watatumia msitu wa Komolo wilayani simanjiro, mtu anayeratibu mafunzo ya wa wanajeshi hao wanafundishwa kwa mwamvuli wa mgambo ni mzee mmoja anaitwa Peter Peshut akishirikiana na Oleleshwa, kwa ufadhili wa kamanda Ndesamburo na Mbowe, naendelea na ufafiti na kuna taarifa kuwa gideon Sanago naye yuko hapa Mererani akiendelea kuwashawishi Apolo wajiunge na jeshi la kina Lema.
 Kada wa CHADEMA akiwa katika gwanda za chadema na Askari akiwa katika gwanda za JWTZ

Huyu msoja nilikua nae jana kwenye mkutano akaniambia yuko tayari kufutwa kazi na kujiunga na makamanda wa Chadema kwasababu anaipenda Chadema na Awezi kujizuia.
Kamanda wa JWTZ akiendelea kusikiliza na kufuatilia mkutano

Pia unaweza bofya hapa ~ http://j.mp/Tje9o9
kusoma maoni ya watu wengine Jamii Forums

No comments:

Post a Comment