Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Tuesday, December 18, 2012

TUSIPOKUWA NA MIKAKATI YA MAANA TUTAENDELEA KUIMBA MILELE TATIZO LA UPUNGUFU WA WALIMU NCHINI.

 
Mhariri.
Kwanza kabisa napenda kuwapongeza kwa kanzi yenu nzuri mnayoifanya kuwahabarisha Watanzania kupitia gazeti hili la Mwananchi, lakini pia ningependa kuwashukuru na kuwapongeza kwa nzuri ya kutuelimisha na makala za miaka 50 ya uhuru katika matoleo mbalimbali ya gazeti hili kusema kweli makala hizo zimetujuza mengi sana . Basi baada ya kutoa pongezi hizo naomba nijikite katika mada yangu iliyonisukuma leo hii nami kujitokeza katika gazeti hili.
Ndugu zangu kwa muda mrefu tumeona wadau mbalimbali hususani serikali ikijisifu kwa jitihada kubwa iliyofanya ya kuongeza shule za sekondari, lakini imekuwa ikadai kuwa changamoto iliyopo mbele yao ni upungufu wa walimu katika shule hizo, na hii imesababisha watu wengi kudhani kuwa katika nchi hii watu waliosomea taaluma ya ualimu ni wachache na hii inachagizwa zaidi na hatua ya serikali kutangaza hatua ya kukabiliana na changamoto hiyo ni kuongeza udahili katika vyuo mbalimbali katika taaluma ya Ualimu na hata kutoa udhamini wa asilimia mia moja kwa wanafunzi wanaosomea ualimu hususani wa Sayansi.
 
Yote haya yanafanywa kwa lengo la kupunguza uhaba wa walimu au kuliondoa kabisa hili tatizo. Lakini mtakubaliana nami kuwa bila ya kuwa na mikakati ya maana hatua zote hizo zitakuwa ni kupotoza muda tu! Na tatizo litaendelea hata baada ya miaka 50 mingine ya uhuru, mathalani, tafiti mbalimbali ambazo zimefanywa na wataalamu na hili linaweza pia kuthibitishwa hata na Maafisa Elimu Sekondari wa Wilaya hapa nchini. Kwanza kati ya wahitimu walimu hususani wa Shahada ni asilimia hamsini tu wanaoripoti vituo vya kazi walivyopangiwa licha ya kupewa mikopo ya silimia mia moja au themanini, wengi wao wanaenda katika ajira nyingine kama vile, polisi, jeshi la wananchi [JWTZ], jeshi la magereza, uhamiaji, wengine katika taasisi binafsi n.k wengine utawakuta hata benki wakifanya kazi lakini ni walimu na wanaokimbilia katika siasa tusiwasahau!
 
Na wale wanaoripoti katika maeneo yao ya kazi wanaripoti kama kutegeshea tu huku wakiendelea kutafuta kazi sehemu mbalimbali wamefanya vituo vyao vya kazi kama sehemu ya kujiegesha tu!
 
Sasa nini kama taifa tunatakiwa kufanya! Ni serikali kuacha kufikiria kushawishi au kuongeza wanafunzi kusomea taaluma ya ualimu na hata kuwadhamini kwa asilimia mia au themanini kwa madai kuwa ualimu ni kipaupembele bila kuboresha maslahi ya walimu hususani mshahara, tukifanya hivyo wanafunzi wenyewe watashawishika kusomea taaluma hii bila hata kuwapa nafauu ya mikopo vyuoni ama vipi. Maana haina maana kusema ualimu ni kipaumbele ukampa mwanafunzi nafuu ya mkopo kwa asilimia zote hizo [100%] bila kujenga mazingira ya mwanafunzi huyo anapohitimu kwenda kufundisha na si kufikiria kazi nyingine zenye maslahi zaidi, hapo itakuwa ni sawa tu na kupoteza pesa tu na muda! Maana hakuna sheria inayombana huyo mwanafunzi kwamba akimaliza lazima akafundishe angalau hata kwa miaka fulani.
 
Ushauri wangu kwa serikali, waangalie namna ya kuboresha maslahi ya walimu, ebu fikiria tu, nesi mwenye cheti [Certificate] mshahara wake anamzidi mwalimu mwenye stashahada ya ualimu we unadhani kwanini watu wasikimbilie huko! Au kazi zinazofanana na hizo! Lakini pia kama inashindwa kuboresha hayo maslahi kwa kiwango kinacholingana na taaluma nyingine kama sheria, uhasibu, madaktari n.k basi wawe wanaingia mikataba maalumu na wanafunzi inaoamua kuwafadhiri kwa asilimia miamoja kwa kozi wanazosema ni kipaumbele kama ualimu, kuwa wataenda kufanya kazi kwa taaluma walizosomea au watakazopangiwa na serikali kwa muda maalumu, hapa inaweza kuwa miaka miwili mitatu au itakayoonekana inafaa. Najua ushauri utakuwa mchungu kwa wanafunzi wanaosomea taaluma fulani kwa ajili ya kupata nafuu ya mikopo utakuwa mbaya kwao, wanisamehe maana NCHI YANGU KWANZA. Kinyume cha hapo tatizo la ualimu utakuwa wimbo wa milele katika taifa letu.


Furaha Venance
Simu: 0715 33 55 558

No comments:

Post a Comment