Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Monday, April 29, 2013

HII NDIYO HATI YA MASHTAKA ALIYOSHITAKIWA NAYO LEMA BAADA YA MENGINE KUFUTWA

 
Kumbuka baadhi ya Mashtaka kabla ya Lema kifikishwa mahakami leo asubuhi, yalikuwa:
 
1. “Dhambi mbaya na kubwa kuliko zote duniani ni woga” na hivyo kuwataka wanachuo wasiwe waoga.
 
 2. Wakati anaongea na wanachuo kuhusu ujio wa mkuu wa mkoa mhe mulongo ambaye alionekana kuchelewa, inadaiwa mhe Lema aliwaambia wanachuo, “NImepata taarifa kuwa ndani ya dakika 15 mkuu wa mkuu atafika, asipofika ndani ya muda huo nitawaongoza kwenda kudai haki yenu ya msingi ya kupatiwa ulinzi.
 
3. Baada ya mkuu wa mkoa kufika aligoma kuongea na wanachuo bila kuwa na kipaza sauti akataka PA system ifungwe ndio aweze kuongea, alipose,a maneno hayo wanafunzi wakaanza kuguna kuwa anaringa, mkuu wa mkoa akasema, kwa hali hii hataweza kuongea na wanafunzi wasio na adabu. Baada ya hapo mhe Lema akasema mbele ya wanachuo, “Hawa ndio viongozi wetu tunaowategemea wanakuja wanajivuta utafikiri wanakwenda kwenye send-off”?.


Hati hiyo ya mashtaka hapo juu, kwa msaada wa Jamii Forums, tembelea hapa https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/442480-hati-ya-mashitaka-ya-mhe-lema-baada-ya-mengine-kutupiliwa.html kusoma maoni ya watu mbalimbali kuhusiana na hati hiyo Jamii Forums

No comments:

Post a Comment