Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Monday, April 29, 2013

MAJIBU YA UV-CCM ARUSHA MJINI KWA HUSSEIN BASHE

Uvccm Wilaya Arusha Mjini

KWA NDUGU YETU HUSSEN BASHE NA WAPOTOSHAJI WENGINE HASWA WA CHADEMA KUHUSU KUKAMATWA KWA LEMA MBUNGE WA ARUSHA MJINI

 
Tangu yalipo tokea mauaji ya kijana mwana chuo wa uhasibu kitendo kilicho pelekea LEMA kukamatwa kwa uchochezi yamesemwa mengi sana kuhusu hili suala na lawama kupewa MH MKUU WETU WA MKOA WA ARUSHA MAGESA MULONGO hatuna malengo ya kumtetea ... mkuu wetu wa mkoa bali kuweka ukweli wazi hapa na kuondoa upotoshaji ambao unafanywa kwa makusudi na baadhi ya wanzetu.
 
 
Suala la kukamatwa kwa Lema mbunge wa Arusha ni kama wanavyo kamatwa wahalifu wengine Lema alifika uhasibu badala ya kupitia kwa viongozi yeye akaenda moja kwa moja kwa wanachuo na kuanza kuwahutubia kitendo ambacho ni utomvu mkubwa wa nidhamu mbunge alipaswa aende ofisini na kuonana na uongozi wa chuo ili apewe taarifa na uongozi wa chuo wampeleke kuongea na wanachuo lakini Lema hakufanya hivyo badala yake alikwenda bila utaratibu na adabu.
 
 
Baada ya Lema kufika na kumaliza kuongea aliyo yaona kuwa ametosheka RC MULONGO alifika na kwasababu uhasibu wanafunzi ni wengi na sauti tunatofautiana aliomba vi pasa sauti ili aweze kuongea na kusikika vizuri hapo kuna dhambi gani mtu kuomba vipasa sauti na vilikuwepo na akapewa ili aongee lakini kwa vile tayari Lema alishaa mwaga sumu tayari walebaadhi ya wanachuo walifanya kama LEMA alivyokuwa amewaelekeza kuwa wafanye fujo.
 
 
Ndugu HUSSEN BASHE kuhusisha kukamatwa kwa LEMA na suala la uchaguzi wa kata nne za ARUSHA mjini hizi ni propaganda ambazo chadema wanazieneza nashangaa na wewe kuwasaidia chadema kufanya propaganda chafu MKUU WA MKOA YEYE NDIYE KIONGOZI WA ULINZI NA USALAMA WA MKOA WETU amekosea wapi kumkamata mwalifu au kukiwepo uchaguzi basi serikali isiwadhibiti wahalifu Bashe post yako uliyo post jana umesukumwa na chuki na wala siyo mapenzi mema NDUGU HUSENI BASHE nawanachadema ambao mmekuwa mkimlaumu mh mkuu wetu wa mkoa kuwa ametumia ubabe sisi kama CHAMA TAWALA TUNARIDHISHWA SANA NA UCHAPAKAZI WA MKUU WETU WA MKOA MAGESA MULONGO kuhusu suala la wauaji kutafutwa lazima watafutwe lakini pia wachochezi na wenyewe ni lazima watafutwe pia maana wote ni tatizo.
 
 
USHINDI WA KATA ZETU NNE UPO NJE NJE BASHE ARUSHA UNAYO ISEMA WEWE KUWA CCM INASHINDWA UMEISOMA MTANDAONI ILA KWA SISI TUNAOISHI ARUSHA WANANCHI WANASEMA WAMETUELEWA nahawako tayari kurudia makosa tena kwa yaliyo tokea wamejifunza Arusha ni mji wakitalii hauhitaji wahuni mwanzo tuliwambia wananchi hawakutuelewa ila kwasasa baada ya kuionja sumu ya CHADEMA wameelewa MKUU WETU WA MKOA VIJANA WA ARUSHA TUKO NA WEWE KATIKA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAKO KW AMUJIBU WA SHERIA BILA KUMWONEA YEYOTE KAMA UNAVYO FANYA ONGERA MAGESA S.MULONGO KWA KUTEKELEZA VYEMA ILANI YETU YA UCHAGUZI
 
 
Afisa habari wa UVCCM wilaya ya Arusha mjini ndugu
SAIDI A. SAIDI

No comments:

Post a Comment