Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Monday, July 29, 2013

MJINI MANYONI, JAMAA AFIA GUEST

Manyoni.
Kijana mmoja ambaye hakuweza kufahamika jina lake amekutwa amefariki katika Nyumba ya kulala wageni hapa mjini Manyoni, mtu huyo ambaye chanzo cha kifo chaka mpaka sasa hakijajulikana, amefia katika nyumba ya kula wageni inayojulikana kwa jina la Luxury Pub ambayo inapakana na Stetionary maarufu ya Calo.
 
Taarifa zaidi zinasema kuwa, wahudumu wa 'guest' hiyo waligundua tukio hilo majira ya saa kumi jioni na kwenda kutoa taarifa Kituo cha Polisi Manyoni ambacho kipo jirani na 'guest' hiyo.
 
Wakati nafika eneo la tukio na polisi ndiyo walikuwa wanatoka na mwili wa marehemu huyo, hadi tunaingia mitamboni haijajulikana kama mtu huyo alikuwa ni mkazi wa Manyoni au alikuwa msafiri na haijajulikana mpaka mauti yanamkuta alikuwa peke yake au na mtu mwingine.

Chanzo: Mimi mwenyewe

No comments:

Post a Comment