Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Sunday, January 13, 2013

HONGERA SUGU! TUKIANZISHA MIFUKO KAMA HII TUNAWEZA KUINUA KIWANGO CHA ELIMU KATIKA MAJIMBO YETU NA WILAYA ZETU

Matokeo mabaya ya mitihani kwa shule zetu za serikali huwa mabaya kwa sababu viongozi wetu waliowengi wamezitelekeza shule hizi. na kama wadau mbalimbali wataamua kuwa na mikakati ya maana tunaweza kuinua kiwango chetu cha elimu katika wilaya zetu, majimbo yetu, mikoa yetu na hata taifa letu kwa ujumla!
 
 
Wapo watu/viongozi ambao kwa namna moja ama nyingine wanajitahidi kubuni na kufanya jitihada mbalimbali ili kuhakikisha wanainua kiwango cha elimu na ufaulu kwa wanafunzi wao, mifano iko, kwa mfano mbunge wa Bumbuli huko Tanga January Makamba ameanzisha mfuko maalum wa elimu jimboni mwake lengo la mfuko huo ni kutoa motisha kwa walimu na wanafunzi wanaofanya vizuri katika jimbo lake.
 
 
mwingine ni mbunge wa Ubongo ndugu John Mnyika naye ameanzisha mfuko wa namna hiyo ukiwa na lengo la kuzisaidia shule, wanafunzi wasiojiweza n.k lakini pia mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi naye ameanzisha mfuko wa namna hiyo pia, na wadau mbalimbali wameweza kujitokeza na kutoa michango yao kwa ajili ya kusaidia katika elimu jimbo hilo la mbeya mjini na kuwasaidia watoto wasio na uwezo!
 
 
je swali la kujiuliza wabunge wengine katika maeneo yetu wanasubiri nini kufanya hivyo? wakuu wa wilaya katika wilaya zao wamefanya nini kusaidia sekta ya elimu katika wilaya zao!
 
 
Je! tunasubiri mpaka rais Kikwete afanye hili katika wilaya zetu/majimbo yetu! watoto wangapi katika wilaya zetu, majimbo yetu, mikoa yetu wanashindwa kuanza na kidato cha kwanza kwa kukosa pesa za kulipa ada, kutengeneza au kununua madawati na michango mingine mingi tu kwa sababu ya umaskini wa wazazi wao?
 
 
walimu na viongozi wa kisiasa wakiamua kushirikiana kwa dhati kabisa tunaweza kuzifanya shule za serikali kuwa kimbilio la watanzania tofauti na hali ilivyo sasa! shule hizi wanasoma watoto ambao wazazi wao hana uwezo wa kuwasomesha katika shule zingine.
 
 
tufanye kama akina Joseph Mbilinyi, kwa mfano leo katika ukurasa wake wa facebook, Mbunge wa mbeya mjini Joseph Mbilinyi  ameandika  kitu kama hiki:
 
 
"SHUKRANI: MH JOSEPH O. MBILINYI (MP),MBUNGE WA MBEYA MJINI NA MWENYEKITI WA MFUKO WA ELIMU MBEYA-(MBEYA EDUCATION TRUST FUND) PAMOJA NA BODI YETU YA WADHAMINI TUNAPENDA KUTOA SHUKRANI ZETU ZA DHATI KWA MAKAMPUNI YAFUATAYO YA MJINI MBEYA KWA KUCHANGIA MFUKO WETU, COCA COLA (5,000,000/-), LAFARGE-MBEYA CEMENT (2, 000, 000/-), TBL (1,OOO,OOO/-) CRDB BANK-MBEYA BRANCH (200,000/-), MWAKIMOMO STORE (150,000/-), NA ACCESS COMPUTERS WALIOTUPATIA COMPUTER MOJA KWA AJILI YA MATUMIZI YA OFISI YA MBETF ILIYOPO KATA YA NZOVWE...
 

 WITO: EWE MWANA-MBEYA NA RAFIKI WA MBEYA POPOTE ULIPO,TAFADHALI CHANGIA MFUKO WA ELIMU ILI TUFIKIE MALENGO YA KUPELEKA SEKONDARI WATOTO WASIO NA UWEZO(UNDERPRIVILEDGED) WAPATAO 360 KWA MWAKA HUU 2013...A/C YETU NI -01J50421214700 CRBD BANK MWANJELWA BRANCH- KWA JINA LA MBEYA EDUCATION TRUST FUND.


TUNATANGULUZA SHUKRANI KWA WOTE WATAKAOTUCHANGIA...
 
Mwisho wa kunukuu. wengine tuige huu mfano. umefika wakati sasa wa kuacha kulaumiana kila mtu atimize wajibu wake kwa nafasi yake na kwa uwezo wake. na hii chini ndo nembo inayotumiwa na huo mfuko wa elimu mbeya [Mbeya Education Trust Fund]
Photo
Kama na wewe katika wilaya yako au jimbo lako kuna mifuko ya aina hii unaweza kutujulisha kwa kuandika hapo chini sehemu ya kuandika comment au kunitumia kwa anuani zetu hapo juu ukitaja jimbo, wilaya jina la mfuko na aliyeuanzisha au anayeusimamia na malengo ya huo mfuko kwa ajili ya kutumia hizo data katika makala yangu nitakayoiandika na kuchapwa katika gazeti la Mwananchi pindi itakapokuwa imekamilika.
 
Imeandikwa na Mwl. Furaha Venance
simu 0715 33 55 58 /0787 33 55 53
 
 
 

No comments:

Post a Comment