Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Thursday, September 12, 2013

HILI SASA BALAA! MWANAMKE AJIFANYA MJAMZITO ABEBA COCAINE KWENYE TUMBO LAKE BANDIA AKAMATWA KIAINA

 
Mwanamke wa Kikanada amekamatwa huko Kolombia akiwa na madawa ya kulevya aina ya cocaine kilo mbili, mzigo huo aliubeba katika tumbo lake bandia akijifanya mama kijacho, Maofisa usalama walimshtukia mkanada huyo, mara baada ya kumuuliza ana mimba ya miezi mingapi? mdada alionekana kama hakulifurahia swali hilo, baada ya muda kidogo akajikuta akijibu kuwa, ana mimba ya miezi saba, jambo ambalo liliwatia wasi wasi vijana 'Saidi Mwema' wa Kolombia, si ndo wakaanza kuichunguza hiyo mimba bwana! Kugusa tumbo, tumbo gumu kama mpira wa miguu! duuh! tumbo lenyewe bwana, likawa la baridi kama limetolewa kwa friji, hapo ndipo msala ukaanza, tazama picha za tukio Zima hapa chini:


Mdada akiwa chini ya ulinzi na katumbo kake bandia
 
Unaliona tumbo lenyewa la miezi saba!
 

Ona tumbo hilo!
 
Latex belly and cocaine that was hidden under it
Tumbo lenyewe hilo kushoto na kulia ndiyo mzigo wenyewe
 
Tumbo lenyewe hilo kushoto na kulia ndiyo mzigo wenyewe
 
 

No comments:

Post a Comment