Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Saturday, September 14, 2013

SUGU AMPONZA AFISA UPELELEZI MKUU WA DODOMA, AHAMISHISHIWA IRAMBA KWA MWIGULU NCHEMBA

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Upelelezi wa Dodoma mjini, Jumanne Amasi, ameingia matatani na kulazimishwa kuhamia Iramba ili yule wa Kiomboi aende Dodoma kuisaidia CCM kukabiliana na wapinzani.
 
Taarifa kutoka chanzo chetu zimethibitisha kuwa mkuu huyo wa upelelezi amehamishwa kwa dharura kwenda Iramba kutokana na shinikizo la kigogo mmoja wa CCM.
 
Hatua hiyo inadaiwa kuwa ni kutokana na mkuu huyo kukataa maelekezo ya kigogo huyo yaliyomtaka amweke mahabusu mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (CHADEMA), baada ya fujo zilizotokea bungeni.
 
Inadaiwa kuwa awali mkuu huyo pia alikataa kumkatama Mbilinyi maarufu kama Sugu alipokuwa Desert Hotel ya mjini Dodoma, akitoa sababu kwa wakuu wake kwamba kosa la mbunge huyo lilitendekea bungeni na alipaswa kuwajibishwa kwa kanuni za Bunge.
 
Alipotafutwa msemaji wa polisi kwa simu kufafanua madai hayo, simu yake iliita bila kupokelewa.
Chanzo chetu kimethibitishiwa na Mkuu wa Upelelezi wa Iramba kuwa tayari amepokea taarifa za kuhamia Dodoma kikazi lakini akadai ni masuala ya kawaida.
Naye mkuu wa upelelezi wa Dodoma, hakuwa tayari kuzungumzia suala hilo kwani alidai kuwa hana taarifa na kwamba kama atahamishiwa Iramba atachukulia kama sehemu ya kazi.
 
Via-Tanzania Daima

No comments:

Post a Comment