Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Monday, October 7, 2013

AL SHABAAB WAUDHIBITI GAROWE BAADA YA KUVAMIWA NA WAMEREKANI

Wanamgambo wa al-Shabab wamedhibiti hali katika mji wa Barawe, ambako makomando wa Marekani walijaribu kumkamata mmoja wa viongozi wa kundi hilo mnamo Jumamosi.
 
Wenyeji wa mji huo wameambia BBC kuwa takriban makomando 200 waliojifunika nyuso zao wamewasili mjini humo wakiwa na silaha nzito.
Inaarifiwa kuwa operesheni ya makomando hao ilikuwa inamlenga raia mmoja msomali kwa jina Abdikadir Mohamed Abdikadir akijulikana kwa jina lengine kama Ikrima.
 
Operesheni hiyo inafanyika baada ya shambulizi la kigaidi nchini Kenya mwezi jana. Al-Shabab, ambayo ni tawi la al-Qaeda, imekiri kutekeleza shambulizi hilo ambalo lilisababisha vifo vya watu 67.
 
 
Hata hivyo maafisa wa eneo hilo bado hawajathibitisha ambako operesheni hiyo ya jumamosi iliyotibuka ilikofanyika
 
 
Siku hiyo hiyo majeshi ya Marekani yalimkamata kiongozi wa Al al-Qaeda Anas al-Liby mjini Tripoli.
 
 
Anashukiwa kuongoza mashambulizi ya kigaidi dhidi ya balozi za Marekani nchini Kenya na Tanzania mwaka 1998 .
 
Wenyeji wanasema kuwa Ikrima ni mmoja wa viongozi wa al-Shabab akiwa na jukumu la kupanga mikakati ya kundi hilo na kuwa huwa amezingirwa na walinzi 20 walio na silaha nzito.
 
Mapema Jumamosi, wanajeshi wa Marekani waliwasili katika nyumba yake karibu na bahari hindi ambako Ikrima hukaa mara kwa mara.
 
Walipokuwa wanaweka ngazi nje ya nyumba, mlinzi alitoa kilio kuhusu watu kuingia katika eneo hilo na kusababisha ufyatulianaji wa risasi uliodumu kwa dakika 20
Wanajeshi hao hata hivyo walirejea baharini na kuingia katika boti zao. Al-Shabab imesema kuwa mmoja wa wapiganaji wake aliuawa wakati wa ukabilianaji huo wa risasi.
 
 
Mwandishi wa BBC Mohammed Moalimu anasema kuwa wenyeji sasa wanahofia kutumia simu zao wasije wakadaiwa kuwa wapelelezi wa Marekani.
 
Al-Shabab imekuwa ikidhibiti eneo hilo tangu mwaka 2008. Walipoulizwa ikiwa serikali ilifahamu kuhusu uvamizi huo, serikali ilisema kuwa ushirikiano wao na washirika wao wa kimataifa kupambana na ugaidi sio siri.
 
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry alisema kuwa harakati dhidi ya ugaidi nchini Libya na Somalia zilionyesha kuwa Marekani kamwe haitachoka kuwachukulia hatua wanaofanya vitendo vya kigaidi.
 
 
Al-Shabab wamelazimia kutoroka miji mikubwa nchini Somalia kwa miaka miwili iliyopita kufuatia operesheni za jeshi la Muungano wa Afrika ingawa bado linadhibiti maeneo mengi ya mashinani.
 
Vi: bbc swahili

No comments:

Post a Comment