Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Saturday, October 12, 2013

MGANGA MKUU HOSPITALI YA MANYONI ATUHUMIWA, MWENYEWE ASEMA NI MAJUNGU TU


KAIMU Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Manyoni mkoani Singida, Dk. Rahim Hangai, amezuiwa kuchukua mafuta lita 2,000 baada ya Mtunza Stoo wa hospitali hiyo, Mary Mayombe, kukataa kusaini vocha inayoruhusu kutolewa mafuta hayo kwa madai kuwa haikufuata sheria.




Akizungumza hivi karibuni na mwandishi wa habari hii, Mayombe alisema alizuia vocha ya lita 2,000 za mafuta kwa sababu ilichukuliwa kinyume cha utaratibu.



Alisema hali hiyo imemsababisha kuondolewa katika nafasi hiyo kutokana na mgongano kati yake na bosi wake.



“Kwa kawaida ili mafuta yatolewe huwa kuna vocha inaandaliwa ambayo inapitia kwangu naisaini ili mtu akapewe mafuta hayo lakini ikiwa inaeleza kila kitu, nikagundua vocha hiyo ina upungufu, nikazuia isiruhusiwe kwenda kwa mzabuni, yaani kituo cha mafuta ambacho ni mzabuni wa hospitali,” alisema.



Alisema yeye ni mwadilifu na mwaminifu katika kazi yake kwani siku zote hufuata sheria za kazi, ndiyo maana alifanikiwa kuzuia hizo lita 2,000 zilizokuwa zitoke kinyume cha utaratibu.



Nao wafanyakazi wa hospitali hiyo walidai kuwa Dk. Hangai alitoa tenda ya kuweka umeme wa jua wenye thamani ya sh milioni 18 bila kufuata taratibu.



Akizungumzia madai hayo, Dk. Hangai alisema tuhuma zote hizo ni majungu na wala hazina ukweli.



“Mwandishi kuhusu suala la mafuta hayo kuna taratibu zake, isingewezekana kuchukua kiasi hicho kikubwa cha mafuta,” alisema.



Alisema hata suala la zabuni ya umeme kuna dosari, kwa kawaida tenda yoyote inayoanzia sh milioni tatu lazima itangazwe gazetini

Chanzo: Tanzania Daima

No comments:

Post a Comment