Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Blog ya kijanja kwa ajili ya watu wajanja

Monday, August 17, 2015

HAYA SASA! MGAWANYO WA MAJIMBO KWA VYAMA VYA UKAWA HUU HAPA, MAJIMBO 12 YAMEBAKI WANAENDELEA NA MAJADILIANO

Ufuatao ni mgawanyo wa majimbo katika kila mkoa Tanzania Bara;-
Mkoa wa Mara
Kwenye mkoa huu majimbo yote tisa wamekabidhiwa Chadema. Majimbo hayo ni Rorya, Tarime Mjini, Tarime Vijijini, Musoma Vijijini, Butiama, Bunda Mjini, Mwibara, Musoma Mjini na Bunda Vijijini.
Mkoa wa Simiyu
Chadema wamegawiwa Jimbo la Bariadi, Maswa Magharibi, Maswa Mashariki, Kisesa, Meatu, Itilima ambapo Busega limekwenda kwa CUF.
Mkoa wa Shinyanga
Majimbo ya Mkoa wa Shinyanga ambayo ni Msalala, Kahama Mjini, Kahama Vijijini, Shinyanga Mjini, Kishapu na Ushetu yamekwenda Chadema.
Mkoa wa Mwanza
Jimbo la Ukerewe, Magu, Nyamagana, Buchosa, Sengerema, , Ilemela, Misungwi yamekabidhiwa Chadema kuhu Jimbo la Kwimba na Sumve wakikabidhiwa CUF.
Mkoa wa Geita
Bukombe, Busanda, Nyang’wale, Chato na Mbogwe yamekwenda Chadema.
Mkoa wa Kagera
Jimbo la Karagwe, Kyerwa, Bukoba Mjini, Muleba Kaskazini, Muleba Kusini, Biharamulo yamekwenda Chadema ambapo Jimbo la Ngara na Nkenge yamekwenda NCCR-Mageuzi na Bukoba Vijijini limechukuliwa na CUF.
Mkoa wa Mbeya
Katika Mkoa wa Mbeya Jimbo la Lupa, Songwe, Mbeya Mjini, Kyela, Rungwe, Busekelo, Mbozi Mashariki, Momba, Mbeya Vijijini, Tunduma na Viwawa yamekwenda Chadema huku Ileje likikabidhiwa kwa NCCR.
Mkoa wa Iringa
Jimbo la Ismani, Kalenga, Mufindi Kaskazini, Iringa Mjini, Kilolo na Mafinga Mjini yamekabidhiwa kwa Chadema ambapo Jimbo la Mufindi Kusini linapiganiwa na NCCR-Mageuzi.
Mkoa wa Dar es Salaam
Jimbo la Ubungo, Kawe, Ukonga, Ilala na Kibamba ni Chadema huku Kinondoni, Temeke, na Mbagala ikielekezwa kwa CUF.
Mkoa wa Njombe
Njombe Kaskazini, Lupembe, Wanging’ombe, Makete, Ludewa na Makambako yamekwenda Chadema.
Mkoa wa Rukwa
Jimbo la Mkasi Kusini, Kwela, Mkasi Kaskazini, Sumbawanga Mjini na Kalambo ni Chadema.
Mkoa wa Tanga
Handeni Mjini, Handeni Vijijini, Pangani, Tanga Mjini, Bumbuli, Mlalo, Lushoto na Mkinga ambapo Korogwe, Muheza, Kilindi na Korogwe Vijijini ni Chadema.
Mkoa wa Kilimanjaro
Jimbo la Rombo, Same Magharibi, Same Mashariki, Moshi Vijijini, Siha, Moshi Mjini na Hai ni Chadema huku Vunjo ikienda kwa NCCR.
Mkoa wa Arusha
Jimbo la Arumeru Mashariki, Arumeru Magharibi, Arusha Mjini, Longido, Monduli, Karatu na Ngorongoro ni Chadema.
Mkoa wa Manyara
Jimbo la Simanjiro, Mbulu Vijijini, Hanang, Babati Mjini, Babati Vijijini, Kiteto na Mbulu Mjini ni Chadema.
Mkoa wa Pwani
Jimbo la Bagamoyo, Kisarawe, Mkuranga, Rufiji Utete, Mafia, Rufiji na Kibiti ambapo Kibaha Mjini, Kibaha Vijijini na Chalinze ni Chadema.
Mkoa wa Morogoro
Jimbo la Kilosa na Morogoro Kusini Mashariki (CUF) ambapo Mikumi, Morogoro Kusini, Kilombero, Mlimba, Mvomero, Ulanga Magharibi, Ulanga Mashariki na Morogoro Mjini ni Chadema.
Mkoa wa Dodoma
Jimbo la Kondoa Mjini, Kondoa Vijijini na Chema ni CUF; Jimbo la Kibakwe na Mtera ni NCCR-Mgeuzi huku Jimbo la Kogwa, Dodoma Mjini, Bahi na Chilonwa yakiwa ni ya Chadema.
Mkoa wa Singida
Jimbo la Iramba Magharibi, Iramba Mashariki, Singida Kaskazini, Singida Mashariki, Singida Magharibi, Manyoni Magharibi na Manyoni Mashariki ni Chadema.
Mkoa wa Tabora
Jimbo la Bukene, Nzega Vijijini, Igalula, Tabora Kaskazini, Kaliua na Tabora Mjini ni CUF ambapo Jimbo la Nzega Mjini, Igunga, Urambo, Ulyankulu, Sikonge na Manonga ni Chadema.
Mkoa wa Katavi
Jimbo la Mpanda Mjini, Mpanda Vijijini, Katavi, Nsimbo na Kavuu ni ya Chadema.
Mkoa wa Kigoma
Buyungu, Mhambwe, Kasulu Mjini, Kasulu Vijijini, Kigoma Kusini, Manyovu (NCCR-Mageuzi) na Kigoma Kaskazini pia Kigoma Mjini ni Chadema.
Mkoa wa Ruvuma
Jimbo la Tunduru Kaskazini, Namtumbo na Tunduru Kusini ni CUF ambapo Mbiga Mjini ni NCCR-Mageuzi. Jimbo la Madaba, Songea Mjini, Mbinga Mashariki/Mbinga, Mbinga Maghribi/Nyasa na Peramilo ni Chadema.
Mkoa wa Mtwara
Jimbo la Newala Mjini, Newala Vijijini, Tandahimba, Mtwara Vijijini, Nanyamba na Nanyumbu ni CUF ambapo Jimbo la Lulindi, Masasi na Ndanda ni NLD.
Mkoa wa Lindi
Jimbo la Mtama, Kilwa Kaskazini, Kilwa Kusini, Lindi Mjini, Ruangwa, Nachingwea, Liwale na Mchinga ni CUF.

Kwa upande wa Zanzibar majimbo yote ya uchaguzi wamekabidhiwa Chama cha Wananchi (CUF) isipokuwa Jimbo la Mkwajuni ambalo wamepewa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

No comments:

Post a Comment